Thursday, May 08, 2014

UTEUZI WA MTENDAJI MKUU WA MAMLAKA YA UDHIBITI NA UNUNUZI WA UMMA (PPRA)

Rais wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt Laurent M. Shirima kuwa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti na Ununuzi wa Umma (PPRA).

Dkt. Shirima ni Mkurugenzi wa kujenga Uwezo wa Huduma za Ushauri (Capacity Building and Advisory Service-PPRA) na pia ndiye anaye kaimu nafasi ya Mtendaji Mkuu wa PPRA.

Kulingana na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, Uteuzi huu umeanza tarehe 2 Mei, 2014.

Imetolewa na;

Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu-Dodoma
Tanzania.

6 Mei, 2014

No comments:

TANZANIA NA URUSI ZAIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI KATIKA SEKTA YA UCHUKUZI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Shirikisho la Urusi zimeingia hatua mpya ya ushirikiano wa maendeleo baada ya kus...