Monday, May 26, 2014

Marais Waondoka Baada ya Kushuhudia Kuapishwa Kwa Rais wa Afrika ya Kusini Jacob Zuma

 Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiondoka Union Buildings baada ya kushuhudia Rais Jacob Zuma akiapa kuwa Rais wa Afrika Kusini kwenye ukumbi wa wazi wa Mandela katika jingo la Union Buildings mjini Pretoria, Afrika Kusini,  Mei 24, 2014
 Marais na viongozi toka nchi mbalimbali wakiondoka Union Buildings baada ya kushuhudia Rais Jacob Zuma akiapa kuwa Rais wa Afrika Kusini kwenye ukumbi wa wazi wa Mandela katika jingo la Union Buildings mjini Pretoria, Afrika Kusini,  Mei 24, 2014.
 Ndege za kijeshi zikiunda umbo la "20" kuashiria miaka ishirini ya uhuru kamili wa Afrika Kusini  katika sherehe za kuapa Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini kwenye ukumbi wa wazi wa Mandela katika jingo la Union Buildings mjini Pretoria, Afrika Kusini,  Mei 24, 2014.Picha na IKULU

No comments: