Wednesday, September 04, 2013

VIFURUSHI VYA AIRTEL YATOSHA VYAZIDI KUBORESHWA ZAIDI


 Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel  Bi, Beatrice Singano Mallya akiongea kuhusu kuboreshwa kwa huduma mpya  ya Airtel Yatosha inayomwezesha mteja wa Airtel kupata kifurushi cha maongezi, sms na internet na kuwasiliana na mitandao yoyote nchini, sasa kwa shilingi 499 mteja anapata dakika 20, sms 300 pamoja na kifurushi cha internet cha 125 MB.

*       Wateja wa Airtel waongezewa dakika za maongezi, SMS na Interneti zaidi katika vifurushi vya Airtel Yatosha

*       Kwa shilingi 499 mteja anapata dakika 20, sms 300 pamoja na kifurushi cha internet cha…

Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel  Bi, Beatrice Singano Mallya akiongea kuhusu kuboreshwa kwa huduma mpya  ya Airtel Yatosha inayomwezesha mteja wa Airtel kupata kifurushi cha maongezi, sms na internet na kuwasiliana na mitandao yoyote nchini, sasa kwa shilingi 499 mteja anapata dakika 20, sms 300 pamoja na kifurushi cha internet cha 125 MB.

*       Wateja wa Airtel waongezewa dakika za maongezi, SMS na Interneti zaidi katika vifurushi vya Airtel Yatosha
*       Kwa shilingi 499 mteja anapata dakika 20, sms 300 pamoja na kifurushi cha internet cha 125MB

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza kuboresha vifurushi vyake vya huduma ya Airtel Yatosha hivyo kuvifanya kuwa bora, vya ushindani na  gharama nafuu nchini.

Akiongea kuhusu kuboreshwa kwa huduma hiyo, Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano Mallya  alisema "huduma ya Airtel Yatosha inaendelea kutosha kuliko yoyote nchini! sasa vifurushi vya Airtel Yatosha vya siku vimeendelea kuboreshwa na kuwa vya gharama nafuu zaidi, kwa shilingi 499 mteja anapata dakika 20, sms 300 pamoja na kifurushi cha internet cha 125MB. Bei ni poa na ya gharama nafuu ukilinganisha na huduma nyingine za vifurushi zinazotelewa sokoni"

Bi. Singano alisema sambamba na hili vifurushi vya Airtel Yatosha vinamuwezesha mteja kupiga simu kwenda mtandao wowote ule nchini wakati wowote masaa 25 yaani mteja anafaidika na vifurushi hivi kwa masaa 24 na 1 la nyongeza siku saba za wiki

Kikubwa na kizuri zaidi mteja anapojiunga na vifurushi hivi anapata nafasi ya kuingia kwenye promosheni yetu kabambe ya Airtel Yatosha Shinda Nyumba na kujishindia pesa taslimu au nyumba  za kisasa zilizoko Kigamboni jijini Dar es saalam"

"Airtel inaendelea na dhamira yake ya kuboresha huduma zake ikiwemo Airtel money yatosha pamoja na vifurushi vya Airtel yatosha vilivyo na gharama nafuu na kukuwezesha kuwasiliana kwa gharama nafuu zaidi ndani na nje ya nchi". aliongeza mmbando

Kujiunga na vifurushi mbalimbali vya Airtel yatosha mteja anatakiwa kupiga *149*99# na kuchagua kifurushi kinachokithi mahitaji yake. Airtel yatosha inapatikana katika  vifurushi vya siku, wiki au mwezi na vifurushi vyake vinadumu kwa masaa 25 kwa siku.



1 comment:

emu-three said...

Kwakweli kifurushi hicho ni kizuri, kinamjali mteja, lakini kuna udhaifi kidogo, mfano, ukijiunga kwa yatisha kwa lengo la inteneti, na zile MB, GB, zikaisha na wakati huo dakika za maongezi bado zipo, huruhusiwi kuongeza yatosha nyingine...sasa kama lengo lako lilikuwa ni internet, inabidi uziangamize zile dakika hewani,..inachukua muda . Twaomba mboreshe na hilo. Pili ukiwa umeweka pesa yako, ili uje ujiunge baadaye na bahati mbaya ukawa kwenye internet, na internet bundle ikawa imekwisha, inakula hadi zile akiba zako ulizoziweka kwa ajili ya kujiunga baadaye bila kupewa taarifa huu sasa sio uungwana. HONGERA NA BORESHENI HILO