Monday, September 23, 2013

BAADA YA MTWARA,LINDI,TANGA NA PWANI SASA KAMPENI YA KUHAMASISHA ULAJI WA VYAKULA VYENYE VIRUTUBISHI WAHAMIA JIJINI DAR ES SALAAM

 Vijana wanaohamasishaji  wa  utumiaji wa vyakula vilivyoongezwa virutubishi wakito elimu hiyo katika mitaa ya Tandika Sokoni  jijini Dar es Salaam, Kampeni hiyo ya uhamasishaji juu ya kuongeza virutubishi kwenye unga wa ngano,unga wa mahindi na mafuta ya kula unazihusisha Wilaya za Kinondoni ,Ilala na Temeke ambapo mlaji anatakiwa kuhakikisha ananunua vyakula  vyenye nembo ya Virutubishi. Kampeni hiyo  inaongozwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia Taasisi ya Chakula na Dawa Tanzaniaz.(TFDA) 
 Wakazi wa Tandika Sokoni jijini Dar es Salaam, wakiwa wamefurika wakati  walipokuwa wakipewa elimu ya  utumiaji wa  vyakula vyenye vitutubishi katika Kampeni inayoendeshwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia Taasisi ya Chakula na Dawa Tanzania.(TFDA)  katika Wilaya za Kinondoni ,Temeke na Ilala.Mbiu ya promosheni hiyo ni kuhakikisha wananchi wanatumia vyakula vywenye nembo ya Virutubishi.
 Akina mama wanaojihusisha na upembuaji wa maharage katika soko la vyakula la Tandika jijini Dar es Salaam,wakimsikiliza kwa makini Adamu Juma   ( kulia) wakati alipokuwa akiwapa elimu ya utumiaji  wa vyakula vilivyoongezwa Virutubishi  .Kampeni hiyo  inaongozwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia Taasisi ya Chakula na Dawa Tanzania.(TFDA) katika  Wilaya za Kinondoni ,Ilala na Temeke ambapo mlaji anatakiwa kuhakikisha ananunua vyakula vilivyowekwa  nembo ya Virutubishi
Wakazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam, wakipata burudani huku pia wakipewa  elimu ya utumiaji  wa vyakula vilivyoongezwa Virutubishi na vijana wa kiundi la black worious wakati wa walipokuwa wakifanyakapeni ya  utumiaji wa vyakula vyenye virutubishi . Kampeni hiyo  inaongozwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia Taasisi ya Chakula na Dawa Tanzania.(TFDA) katika  Wilaya za Kinondoni ,Ilala na Temeke ambapo mlaji anatakiwa kuhakikisha ananunua vyakula vilivyowekwa nembo ya Virutubishi.

No comments: