Tuesday, August 23, 2011

Mbunge Silima aliyenusurika jana afariki dunia

Marehemu mbunge Silima

MBUNGE mteule kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mussa Khamis Silima, ambaye alipata ajali juzi katika aneo la Nzuguni, Dodoma, amefariki dunia leo. Pichani juu: Marehemu akiwa katika machela baada ya kushushwa kwenye gari juzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam, alikoletwa na ndege kutoka Dodoma pamoja na gari alilopata nalo ajali. Mke wa marehemu, Mwanaheri Fahari nae alifariki katika ajali hiyo na kuzikwa jana na dereva wao Chezani Sebunga alijeruhiwa.

No comments:

RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...