Tuesday, August 23, 2011

Mbunge Silima aliyenusurika jana afariki dunia

Marehemu mbunge Silima

MBUNGE mteule kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mussa Khamis Silima, ambaye alipata ajali juzi katika aneo la Nzuguni, Dodoma, amefariki dunia leo. Pichani juu: Marehemu akiwa katika machela baada ya kushushwa kwenye gari juzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam, alikoletwa na ndege kutoka Dodoma pamoja na gari alilopata nalo ajali. Mke wa marehemu, Mwanaheri Fahari nae alifariki katika ajali hiyo na kuzikwa jana na dereva wao Chezani Sebunga alijeruhiwa.

No comments:

SERIKALI YATOA MAELEKEZO NANE KUIMARISHA KAMPUNI AMBAZO INA UMILIKI HISA CHACHE KUELEKEA DIRA 2050

Arusha. Serikali imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni ambazo ina umiliki wa hisa  chache, ikiwa ni ...