Wednesday, August 17, 2011

Dk Shein atembelea wizara mbalimbali


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo, katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar, akiwa katika mfululizo wa ratiba zake za kuzungumza na kila Wizara, katika kuhakikisha kila taasisi za wizara hiyo inatekeleza majukumu yake.

Rais wa Zabziar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk Ali Mohamed Shein,akizungumza na uongozi wa Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo,katika mkutano uliojadili mambo ya utekelezaji wa majukumu ya wizara hiyo ambayo yataweza kukuza uchumi wetu na kuwaletea maendeleo wananchi,(kushoto) Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi.

Rais wa Zabziar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk Ali Mohamed Shein,akifuatari na Uongozi wa Benki ya watu wa Zanzibar,PBZ,uliomualika Rais katika futari iliyowashirikisha baadhi ya wananchi mbali mbali katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort leo.

Baadhi ya Wananchi na wafanya biashara mbali mbali wakifutari kwa pamoja pia akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk Ali Mohamed Shein,pamoja na Uongozi wa Benki ya watu wa Zanzibar,PBZ,ulioyarisha futari hiyo ikiwa ni kila mwaka huwaalika watu mbali mbali katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort.

Rais wa Zabziar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk Ali Mohamed Shein, akitia chakula cha futari iliyoandaliwa na Uongozi wa Benki ya watu wa Zanzibar, PBZ, wakati aliposhiriki pamoja na viongozi wengine pia wakiwemo wafanya biashara mbali nbali, katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort leo. Picha na Ramadhan Othman Ikulu.

No comments: