Wednesday, August 10, 2011

Kizaazaa cha mafuta: Serikali yatoa tamko rasmi, BP, Engen, Oilcom na Camel Oil matatani


Mkurugenzi wa Mamlaka ya udhibiti wa Nishati ya maji na mafuta(EWURA) Haruna Masebo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu maamuzi ya serikali yaliyofikia katika kutatua tatizo la mgomo wa wauuzaji wa mafuta.Picha na Fidelis Felix

EWURA imetoa Compliance Order ( amri ya kutii amri) kwa makampuni manne ambayo ni BP, Engen, Oilcom na Camel Oil, ambapo wanatakiwa watekeleze hatua zifuatazo:

1. Mara moja wanatakiwa kuanza kutoa huduma katika maghala yao ikiwa ni pamoja na kuanza kuuza mafuta katika vituo vya rejareja ikiwemo vituo vilivyo chini ya miliki zao;
2. Waache mara moja kitendo chochote kitakachosababisha upungufu wa makusudi wa mafuta ya petroli katika soko la Tanzania; na
3. katika kipindi cha masaa 24 wajieleze kwa nini wasichukuliwe hatua za kisheria dhidi yao kwa kukiuka matakwa ya Sheria ya Mafuta pamoja na Sheria ya EWURA.
Hebu cheki http://michuzi-matukio.blogspot.com/2011/08/tamko-la-waziri-wa-nishati-na-madini.html#links

No comments: