Tuesday, June 02, 2009

Baba wa taifa Guinea Bissau aaga dunia


Luis Cabral ambaye aliiongoza Guinea-Bissau mara baada ya kupata uhuru amefariki dunia akiwa nchini Ureno ambako amekuwa akiishi kama mkimbizi tangu kutimuliwa madarakani mwaka wa 1980.

Bwana Cabral ambaye alichukuwa wadhifa wa urais mnamo mwaka wa 1974 aling’olewa madarakani na Joao Bernardo Vieira ambaye aliuawa mwezi Machi mwaka huu.

Kabla ya kuhamia mjini Lisbon, Ureno, Bwana Cabral alikimbilia Cuba.

Taarifa ya serikali ilisema, “Serikali na wananchi wa Guinea-Bissau wanasikitika kutangaza kifo cha mpendwa Luis Cabral.”

Serikali inatarajiwa kuandaa kikao cha dharura kuandaa siku tatu za maombolezo ya kitaifa.
Habari kutoka BBC.

No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...