Thursday, June 11, 2009

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Sukita mzee John Kapinga azikwa

Mke wa rais mama Salma Kikwete akiweka shada la maua juu ya kaburi la ndugu John Kolos Kapinga wakati wa mazishi ya aliyekuwa mkurugenzi wa SUKITA ndugu John Kolos Kapinga yaliyofanyika nyumbani kwake eneo la Kimara stop over jijini Dar es salaam.
Mapadre wa kanisa Katoliki Parokia ya Mavurunza wakiongozwa na Paroko wa kanisa hilo Erasto Nyoni wakati wa ibada ya mazishi ya marehemu John Kolos Kapinga.Marehemu Kapinga alizikwa jana jioni nyumbani kwake eneo la Kimara stop over, Dar es salaam.
Mke wa marehemu John Kapinga akiweka udongo kwenye kaburi la mumewe marehemu Kapinga wakati wa mazishi yaliyofanyika jana jioni eneo la Kimara stop over jijini Dar es salaam.
Ndugu , jamaa na watoto wa aliyekuwa Mkurugenzi wa SUKITA marehemu John Kolos Kapinga wakiwa mbele ya kaburi la John Kapinga wakiongozwa na mke wa marehemu mama Revy Kapinga (wa pili kulia mstari wa mbele)

Mama Revy Kapinga akiweka shada la maua juu ya kaburi la mumewe marehemu John Kolos Kapinga wakati wa mazishi yaliyofanyika jana jioni eneo la Kimara stop over jijini Dar es salaam.Picha zote zimepigwa na mdau Aron Msigwa wa MAELEZO- Dar.

No comments: