Monday, June 22, 2009

nasma khamis afariki dunia


Mwimbaji mahiri na aliyewahi kutamba sana kwenye anga ya muziki wa taarabu hapa nchini,Bibie Nasma Khamis wa Kidogo (shoto pichani) amefariki dunia usiku wa kumkia leo, kutokana na taarifa ambazo si rasmi sana Jiachie imezipata zinaeleza kuwa msiba huo upo Kinondoni,Jijini Dar.Kwa habari kamili tega sikio hapa hapa Jamvini.
Nasma Khamis 'Kidogo' (shoto) enzi za uhai wake na Bi Khadija Omar Kopa wakila pozi pamoja. Malkia hawa wa taarab ya kisasa inayonakshiwa kwa mipasho, walikuwa ni wahasimu wakubwa jukwaani na marafiki wa karibu mitaani. Taarifa hizi ni kwa mujibu wa http://michuzijr.blogspot.com/2009/06/nasma-khamis-afariki-dunia.html#comments

BUNGE LAMTHIBITISHA NDEJEMBI KWA ASILIMIA 100 UMAKAMU WA RAIS.

Waziri Mkuu asema anatosha, kiti kimempata mtu sahihi wa kumsaidia Mheshimiwa Rais. BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo (Ijumaa, Ag...