Monday, June 22, 2009

nasma khamis afariki dunia


Mwimbaji mahiri na aliyewahi kutamba sana kwenye anga ya muziki wa taarabu hapa nchini,Bibie Nasma Khamis wa Kidogo (shoto pichani) amefariki dunia usiku wa kumkia leo, kutokana na taarifa ambazo si rasmi sana Jiachie imezipata zinaeleza kuwa msiba huo upo Kinondoni,Jijini Dar.Kwa habari kamili tega sikio hapa hapa Jamvini.
Nasma Khamis 'Kidogo' (shoto) enzi za uhai wake na Bi Khadija Omar Kopa wakila pozi pamoja. Malkia hawa wa taarab ya kisasa inayonakshiwa kwa mipasho, walikuwa ni wahasimu wakubwa jukwaani na marafiki wa karibu mitaani. Taarifa hizi ni kwa mujibu wa http://michuzijr.blogspot.com/2009/06/nasma-khamis-afariki-dunia.html#comments

KIPANGULA: WAHITIMU WA HABARI WATAFAIDIKA NA MABORESHO YA KANUNI

  Na Mwandishi Wetu Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amewashauri Waandishi ...