Monday, June 22, 2009

nasma khamis afariki dunia


Mwimbaji mahiri na aliyewahi kutamba sana kwenye anga ya muziki wa taarabu hapa nchini,Bibie Nasma Khamis wa Kidogo (shoto pichani) amefariki dunia usiku wa kumkia leo, kutokana na taarifa ambazo si rasmi sana Jiachie imezipata zinaeleza kuwa msiba huo upo Kinondoni,Jijini Dar.Kwa habari kamili tega sikio hapa hapa Jamvini.
Nasma Khamis 'Kidogo' (shoto) enzi za uhai wake na Bi Khadija Omar Kopa wakila pozi pamoja. Malkia hawa wa taarab ya kisasa inayonakshiwa kwa mipasho, walikuwa ni wahasimu wakubwa jukwaani na marafiki wa karibu mitaani. Taarifa hizi ni kwa mujibu wa http://michuzijr.blogspot.com/2009/06/nasma-khamis-afariki-dunia.html#comments

KASI YA UJENZI WA RELI YA SGR IMEONGEZEKA – PROF. MBARAWA

  Wahudumu wa ndani (Train crew) wa shirika la reli Tanzania (TRC) upande wa Standard Gauge Railway (SGR) wamehudhuria Bungeni Jijini Dodoma...