Saturday, June 27, 2009

kaimu mufti sheikh Gorogosi afariki dunia


Kaimu Mufti wa Tanzania Sheikh Suleiman Gorogosi amefariki dunia leo mchana baada ya kupata ajali katika kijiji cha Mnolela mkoani Lindi.

Akizungumza na globu hii mkuu wa mkoa wa Lindi Said Meck Sadick amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo majira ya saa saba na robo mchana.

Taarifa zilizopatikana baadaye zinasema kwamba Kaimu mufti ambaye pia ni Sheikh wa mkoa wa Lindi alikuwa anasafiri kutoka katika mji wa Mtwara ambako alishuka na ndege kuelekea Lindi mjini.

Habari zaidi zinasema kwamba bakwata wanaandaa mpango wa maziko ya kiongozi huyo wa bakwata.

No comments:

RAIS SAMIA AFUNGUA SOKO LA KISASA KARIAKOO LILILOGHARIMU BILIONI 28, SASA BIASHARA SAA 24

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Sok...