Saturday, June 27, 2009

kaimu mufti sheikh Gorogosi afariki dunia


Kaimu Mufti wa Tanzania Sheikh Suleiman Gorogosi amefariki dunia leo mchana baada ya kupata ajali katika kijiji cha Mnolela mkoani Lindi.

Akizungumza na globu hii mkuu wa mkoa wa Lindi Said Meck Sadick amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo majira ya saa saba na robo mchana.

Taarifa zilizopatikana baadaye zinasema kwamba Kaimu mufti ambaye pia ni Sheikh wa mkoa wa Lindi alikuwa anasafiri kutoka katika mji wa Mtwara ambako alishuka na ndege kuelekea Lindi mjini.

Habari zaidi zinasema kwamba bakwata wanaandaa mpango wa maziko ya kiongozi huyo wa bakwata.

No comments:

MMUYA: WANANCHI WANUFAIKE NA UWEKEZAJI WA NHC KUPITIA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, amekagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa maghala unaotekelezwa na S...