Saturday, June 27, 2009

kaimu mufti sheikh Gorogosi afariki dunia


Kaimu Mufti wa Tanzania Sheikh Suleiman Gorogosi amefariki dunia leo mchana baada ya kupata ajali katika kijiji cha Mnolela mkoani Lindi.

Akizungumza na globu hii mkuu wa mkoa wa Lindi Said Meck Sadick amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo majira ya saa saba na robo mchana.

Taarifa zilizopatikana baadaye zinasema kwamba Kaimu mufti ambaye pia ni Sheikh wa mkoa wa Lindi alikuwa anasafiri kutoka katika mji wa Mtwara ambako alishuka na ndege kuelekea Lindi mjini.

Habari zaidi zinasema kwamba bakwata wanaandaa mpango wa maziko ya kiongozi huyo wa bakwata.

No comments:

RUZUKU YA SH.MILIONI 250 YATOLEWA KWA WABUNIFU WA MATUMIZI BORA YA NISHATI

📌 Kamishna wa Umeme asema Serikali itaendelea kuwawezesha vijana wabunifu katika teknolojia ya matumizi bora ya nishati 📌 Wabunifu wa kike...