Tuesday, January 01, 2008

Wazungu wamkalia kooni Kibaki

ULE ujanja wa kishetani uliofanywa na Mwai Kibaki, Rais wa Kenya aliyejinyakulia uongozi wa kutangazwa na hatimaye kuapishwa umeanza kumtokea puani baada ya mataifa ya Magharibi kupinga matokeo ya kura za uchaguzi wa Kenya yaliyompa ushindi kuongoza nchi hiyo katika kipindi kingine cha miaka mitano.

Waangalizi wa Kimataifa kutoka Jumuhia ya Ulaya wametoa tamko lao na kuelezea uchaguzi huo ulikuwa na kasoro kubwa.
Waangalizi hao walisema kuwa Rais wa Kenya hakupatikana kihalali na kwamba matokeo hayo hayakukidhi viwango vya kimataifa. Soma habari hii katika shirika la AFP kwa taarifa zaidi.

No comments:

RUZUKU YA SH.MILIONI 250 YATOLEWA KWA WABUNIFU WA MATUMIZI BORA YA NISHATI

📌 Kamishna wa Umeme asema Serikali itaendelea kuwawezesha vijana wabunifu katika teknolojia ya matumizi bora ya nishati 📌 Wabunifu wa kike...