CHAMA kikuu cha upinzani nchini Kenya cha Orange Democratic Movement (ODM), kimepanga kufanya maandamano makubwa ya siku tatu mfululizo kupinga matokeo yaliyomtangaza Rais Mwai Kibaki kuongoza tena katika kipindi kingine cha miaka mitano ijayo.
Tangazo hilo linafuatia juhudi za kimataifa za kutaka suluhu baina ya pande mbili zinazovutana zilizofanywa na Mwenyekiti wa Muungano wa Afrika (AU), ambaye ni Rais wa Ghana, John Kufuor kushindikana.
Raisi Kufuor aliondoka mjini Nairobi juzi huku akishindwa kukutana na kufanya mazungumzo hayo ya kuleta amani baina ya Raila Odinga na Rais Mwai Kibaki.
Mpaka sasa zaidi ya watu wanaokadiriwa kufikia 600 wameripotiwa kupoteza maisha katika ghasia hizo zilizotokea katika sehemu mbalimbali ya nchi hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
MMUYA: WANANCHI WANUFAIKE NA UWEKEZAJI WA NHC KUPITIA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, amekagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa maghala unaotekelezwa na S...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Nadhani mtakumbuka kibwagizo maarufu katika TV ambacho kinaimbwa perupe pepero perupe pepero hawa ni vijana wa Sisi Tambala waliokuwapo kati...
No comments:
Post a Comment