Saturday, January 19, 2008

Kanumba ndani ya Hollywood



Mcheza sinema maarufu wa Tanzania, Steven Kanumba aka. Denzel wa Tanzania, yuko ziarani Marekani. Kwa sasa yuko Hollywood. Ametembelea Warner Brothers na Universal Studios.

Juzi juzi kapewa tuzo ya Best Tanzania Hollywood Achievement, kutoka Kampuni ya Universal Hollywood ya nchini humo.
Hii ni tuzo ya pili kwa msanii huyo kutunikiwa kutoka Marekani ambapo ya kwanza ni ya Johnwyne International Award.

Kanumba yuko nchini Marekani kwa takriban miezi mitatu sasa kwa mwaliko wa Kampuni ya Johnwyne ya Hollywood.

Bonyeza hapatu upate habari zaidi.

1 comment:

Anonymous said...

Kanumba hajapata John Wayne International Award wala Award kutok Universal Studios. Hakuna awards kama hizo! Hiyo ni toy aliyonunua kwenye duka la watalii. Jamani anawafanya wabongo watoto wadogo.

MAJALIWA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA TEWW

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Oktoba 25, 2025 ni mgeni rasmi katika kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Taasisi ya Elimu y...