Wednesday, August 30, 2017

WANAFUNZI MSALATO GIRLS WAJIPANGA KUINGIA 10 BORA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua maeneo ya vyoo na mifumo ya maji iliyokarabatiwa katika shule ya Sekondari ya wasichana Msalato.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akipata maelezo ya ukarabati wa mabwene kutoka kwa mmoja wa wakandarasi wanaofanya ukarabati huo.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akifanya ukaguzi wa mabweni nane yaliyofanyiwa ukarabati katika shule ya Sekondari ya wasichana.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na Mkuu wa shule hiyo pamoja na maafisa wengine wakifanya ukaguzi wa majengo.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Msalato Dodoma.
Miongoni mwa mabweni yaliyokarabatiwa na serikali.

Wanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya sekondari ya wasichana ya Msalato Manispaa ya Dodoma wamemuahidi Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Mhe. Selemani Jafo kwamba watapambana ili katika matokeo ya kidato cha sita mwakani shule yao iwe miongoni mwa shule kumi bora nchini. 

Ahadi hiyo ilitolewa na wanafunzi hao katika ziara ya Naibu Waziri Jafo alipotembelea shule hiyo kukagua ujenzi wa miundombinu inayojengwa na serikali ili kuirudisha shule hiyo katika hadhi yake.

Shule hiyo ni miongoni mwa shule kongwe 88 zilizo katika mpango wa ukarabatiwa na serikali ambapo ndani ya miaka 4 shule hizo zitakuwa ni shule zenye ubora wa hali ya juu kwa kuboreshewa mazingira yake yakiwemo mabweni, madarasa, vyoo, mabwalo, mifumo ya maji na umeme, pamoja na nyumba za walimu. 

Katika shule hiyo, serikali hadi sasa imeshakamilisha ukarabati wa mabweni nane, mfumo wa umeme na maji.Aidha Serikali imejipanga kuendelea na ukarabati wa madarasa na ujenzi wa madarasa mengine manne mapya, ukarabati wa bwalo la chakula, majengo ya utawala, na nyumba za walimu. 

Kufuatia uboreshaji huo, Wanafunzi wameishukuru serikali na wamemuahidi Naibu Waziri huyo kwamba watahakikisha wanajitahidi ili mwakani shule yao iwe miongoni mwa shule kumi bora katika matokeo ya kidato cha sita.

Akizungumza na wanafunzi hao, Naibu Waziri Jafo amewahakikishi watanzania kwamba mpango wa serikali ni kuboresha shule za umma ili ziweze kutoa elimu bora hapa nchini.Mwaka jana, Naibu Waziri Jafo alitembelea shule hiyo na kuwataka wanafunzi wa kidato cha sita kuhakikisha wanafanya vizuri katika mitihani yao ili shule hiyo itoke kutoka shule ya 21 katika matokeo ya kidato cha sita mwaka jana ili waingie 10 bora. Jambo ambalo katika matokeo ya mwaka huu shule hiyo imeshika nafasi ya namba 14 kitaifa.

No comments: