Thursday, August 31, 2017

Kamati za kudumu za bunge za Pac na Laac zaendelea na vikao vyake leo Mjini Dodoma

1
 Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Mussa Mbaruku akizungumza jambo pale kamati hiyo ilipokutana na viongozi kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, kwa lengo la kuwapitisha Wajumbe wa kamati kuhusu hesabu za fedha za Taasisi husika, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Dodoma. kulia ni Mjumbe wa kamati hiyo Mhe. Juma Aweso
2
 Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Japhet Hasunga akiongoza kikao cha kamati hiyo pale  ilipokutana na viongozi kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, kwa lengo la kuwapitisha Wajumbe wa kamati kuhusu hesabu za fedha za Taasisi husika, katika kikao kilichofanyika leo Mjini Dodoma.
3
 Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wakifuatilia mazungumzo baina yao na Viongozi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi lengo likiwa ni kupitia Mahesabu na Maagizo ya kamati hiyo, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Dodoma kikiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Naghenjwa kaboyoka(katikati).
4
Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) Mhe. Vedasto Ngombale (katikati) akiongoza kikao cha kamati hiyo dhidi ya viongozi kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Hazina na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) katika kikao kilichofanyika jana Mjini Dodoma.kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Abdallah Chikota na kulia ni katibu kamati wa Bunge, Ndg. Dismiss Muyanja


(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments: