Tuesday, October 30, 2012

SIKU YA IBADA YA KUOMBEA AMANI KWA TAIFA MCH. DK RWAKATARE AIBUKA NA UJUMBE MZITO

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni Mh. Dkt. Getrude Rwakatare akitoa Ujumbe kwa Watanzania waliohudhiria Ibada Maalum ya Kuliombea Taifa ambapo ametaka watu kutobaguana kwa misingi ya Dini, Ukabila wala Siasa na kusema pamoja na Utawala bora pia tunahitaji maombezi ili tuweze kufikia Malengo yaliyokusudiwa kulipeleka Taifa linapotakiwa kufikia.
Dkt. Rwakatare amesema nia kubwa ya kufanya Ibada hiyo ya Maombezi ni kutaka kuweka usawa kutokana na siku za hivi karibuni kuibuka kwa Matamko mbalimbali kutoka kwa watu tofauti wakiwemo viongozi wa Kitaifa, Kidini na wa baadhi ya Makundi yanayohitilafiana na kusema tukiomba kwa jina la Mungu kila kitu kitakwenda kama tulivyomuomba ili Tanzania iendelee kuwa nchi ya Amani na Utulivu kama ilivyokuwa miaka yote ambayo ni kimbilio la watu wa Mataifa mbalimbali kwa sababu Watanzania hawajui kuchukiana na wamekuwa watu wa kushikamana kwa miaka yote.
Picha Juu na Chini ni Waumini waliohudhiria Ibada Maalum ya kuliombea Taifa wakinyanyua bendera juu kuimba na kuabudu kwa furaha bila kuonyesha tofauti ya matabaka.
Msanii wa Kimataifa wa muziki wa nyimbo za Injili wa Tanzania Rose Muhando akiimba na kumtukuza Mungu sambamba na wachezaji wake wakati wa Ibada hiyo maalum ya kuliombea Taifa letu liendelee kuwa na Amani, Upendo na Utulivu.
Nimeonja Utamu wa Yesu Weeeeee........!!!
Mchungaji Kiongozi Dkt. Rwakatare akijumuika sambam

No comments: