Saturday, October 13, 2012

RPC Mwanza auawa kwa Kupigwa Risasi na Majambazi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow ameuawa kwa kupigwa risasi na majambazi usiku wa kuamkia leo katika maeneo ya Kitangiri jijini Mwanza.

Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Said Mwema amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kusema timu ya Makachero kutoka Dar ikiongozwa na Mkurugenzi wa Upepelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba inakwenda jijini humo kuongeza nguvu ya kiupelelezi na taarifa zaidi zitatolewa baadaye.
R.I.P KAMANDA LIBERATUS BARLOW 

No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...