Monday, October 22, 2012

WAENDA UINGEREZA KUONA BARCLAYS PREMIER LEAGUE

Tunu Kavishe, (Katikati), Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano benki ya Barclays-Tanzania, akizungumza muda mfupi kabla ya kuchezeshwa bahati nasibu ya promosheni ya Barclays ya shinda na ukaone ligi kuu ya Uingereza,  Katika bahati nasibu hiyo, mteja wa benki hiyo jijini Mbeya, Anthony Hancy, aliibuka mshindina hivyo kujipatia nafasi ya kusafiri kwenda uingereza akiwa na ampendaye ili kujionea ligi kuu ya nchi hiyo maarufu kama, "Barclays Premier League". 

Afisa Mawasiliano wa benki ya Barclays, Lillian akichagua kikaratasi wakati wa kuchezeshwa kwa bahati nasibu hiyo iliyosimamiwa na mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha, Bakar Majjid, (Kulia). Bahatinasibu hiyo ilichezeshwa Jumatatu Oktoba 22, 2012 kwenye tawi la benki hiyo, Kijitonyama jijini Dar es salaam

No comments:

WIZARA YA AFYA YAOMBA SH. TRILIONI 1.8 BAJETI YA 2026/2027

  Wizara ya Afya imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma z...