Tuesday, September 08, 2009

Makumbusho ya zama za mawe za kale za Isimila hatarini kutoweka









ZAMA za mawe za kale na nguzo za asili za Isimila zilizo katika kijiji cha Ugwachanya, ni miongoni mwa Vivutio vinavyoupamba Mkoa wa Iringa.
Zama hizo zinakadiliwa kuishi miaka laki tatu hadi laki nne kabla ya kristo, na ziligunduliwa na wenyeji wa eneo hilo kabla ya kufanyika utafiti mwaka 1951 kisha eneo hilo kutangazwa rasmi kwamba lina utajiri wa masalia ya zama hizo .
Miongoni mwa zama zilizo katika Korongo la Isimila lenye mikondo miwili, ni Mikuki iliyotumika kwa ajili ya kujihami na mawe ya kombea kwa ajili ya kazi ya uwindaji.
Nyundo zilizokuwa zikitumika kwa ajili ya kutengenezea zama nyingine na Shoka mahususi kwa kazi ya kuvunja mifupa, Vyembe na visu. Taarifa ya Tumaini Msowoya.

No comments:

RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...