Wednesday, November 02, 2016

THE FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY WAJIPANGA KUADHIMISHA JUMANNE YA KUTOA (GIVINGTUESDAY) KWA KUWASAIDIA WATOTO NDANI YA SHULE YA WALEMAVU YA UHURU MCHANGANYIKO



Foundation for civil society ambao ni asasi huru imetangaza kutumia utaratibu wa JUMANNE YA KUTOA (GIVINGTUESDAY) utaratibu ambao unatumika duniani kote kwa ajili ya kuhamasisha watu na jamii kuwa na moyo wa kujitolea kwa ajili ya wahitaji ambapo asasi hiyo imetangaza kuadhimisha siku hiyo hapa nchini kwa kuwasaidia watoto wenye ulemavu wanaosoma katika shule ya msingi Uhuru mchanganyiko ikiwa ni mara ya kwanza kwa Asasi hiyo kuadhimisha siku hiyo muhimu.
Akizungumza na mtandao huu katika mahojiano maalum leo Martha Olotu ambaye ni Busness,Development and Partinaship Manager wa Asasi hiyo amesema kuwa FCS inalenga kutumia Utaratibu wa Jumanne ya Kutoa kwa namna ya kuhamasisha Moyo wa kujitolewa kwa wenye Uhitaji,ikiwa ni Jitihada za ulimwengu ambazo zilizinduliwa Rasmi Tangu mwaka 2012 na shirika la New York’s 92nd streat Y kwa ushirikiano na UN Foundation,Lengo likiwa ni kuweka siku maalum kwa ajili kuheshimu na kuadhimisha ukarimu katika kutoa,ambapo kwa sasa siku hii imekuwa ikiadhimishwa na nchi nyingi Duniani ikihusisha makampuni Binafsi,watu binafsi,familia na asasi za kiraia.



Akizungumzia maadhimisho hayo ambayo yatafanyika Tarehe 29 mwezi wa November Karin Rupia Ambaye Ni Resource Mobilization Executive Kutoka katika asasi hiyo amesema kuwa shirika hilo litakabidhi michango iliyotolewa, na kujiunga kufurahi na watoto kwenye shughuli kama kupima afya za watoto hao,kuchora na watoto,kucheza na watoto kusafisha watoto pamoja na kuwasomea watoto hao wa shule ya msingi Uhuru mchanganyiko.

Kwa maelezo zaidi Juu ya siku hiyo unaweza kutizama HABARI24 TV kwenye Youtube account yetu hapo.

No comments: