Monday, November 21, 2016

Hii Ndiyo Stendi Mpya ya Mabasi Msamvu, Baada ya Kukarabatiwa, Sasa Inang’aa Kama Airport!

msamvu-1Upande wa kuingilia abiria kwenye stendi hiyo.
msamvu-2Abiria wakisubili usafiri.
msamvu-3Moja ya mabasi hayo likiingia eneo la stendi na kupakia na kushusha abiria.msamvu-4Muonekano wa mbele wa stendi hiyo. msamvu-5Pia kama huna tiketi kuingia kwenye stendi hiyo utarazimika kulipia Tsh. 200, ichani mmoja wawafanyakazi wa stendi hiyo akikusanya pesa hizo.msamvu-6Basi la Kisbo baada ya kushusha na kupakia abiria lilikaguliwa na polisi kisha kuruhusiwa kutoka kwenye geti la stendi hiyo na kuendelea na safari. msamvu-7msamvu-8msamvu-9Mmoja wa mawakala wa mabasi kwenye stendi, Ayubu akisaka abiria.msamvu-10Bustani zikichanua.
msamvu-11Muonekano wa nyuma wa stendi hiyo kulia mwenye T-shirt ya Bluu Jumanne Mtangwa beki wa zamani wa Klabu ya Reli ya Morogoro ‘Kiboko ya Vigogo’ ambaye kwa sasa ni mpiga-debe kwenye stendi hiyo akimuongoza mwandishi wetu kumuonesha maeneo mbalimbali ya stendi hiyo.
msamvu-12
Na Dustan Shekidele, Morogoro.
HATIMAYE baada ya ukarabati wa takribani miaka miwili, hatimaye Stendi ya Mabasi ya Mikoani ya Msamvu iliyopo Morogoro imefunguliwa mwishoni mwa wiki iliyopita huku ikiwa na muonekano wa kisasa kabisa na wengine kuifananisha na uwanja wa ndege ‘Airport’.
Leo asubuhi tovuti yetu imetinga ndani ya stendi hiyo ya kisasa ambayo iko kwenye hatua za mwisho za kumalizia ukarabati kwa kiwango cha hali ya juu, ambapo picha zilizopigwa zinaonesha namna ambavyo mandhari ya stendi hiyo yanavyovutia kwa sasa tofauti na ilivyokuwa awali kabla ya ukarabati.
Wameshuhudiwa abiria wengi wakipanda na kushuka kwenye mabasi kama wako uwanja wa ndege huku wengine wakisubili usafiri ili kuelekea sehemu mbalimbali.
Akizungumza na mwandishi wetu, mmoja wa viongozi wa Stendi hiyo, ameeleza kuwa, endapo wakimkamata mtu yoyote akitupa takataka ama kukanyaga bustani atatozwa faini ya Tsh. 50,000/= papo hapo.

No comments: