Tuesday, November 01, 2016

JESHI LA POLISI LINAWASHIKILIA WATU 200 KWA MAKOSA MBALMBALI

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro akionyesha panga ambazo wamezikamata katika operesheni  jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro akionyesha gari la Polisi likiwa linabeba mzigo wa bangi uliokatwa na Polisi katika msako ulifanyika jijini Dar es Salaam. 


Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari juu ya operesheni walizozifanya hivi karibuni  jijini Dar es Salaam. 
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro akionyesha bunduki ambayo iliangushwa na wtu wanaodhaniwa kuwa majambazi  jijini Dar es Salaam. 
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro akionyesha kwa waandishi habari begi la bangi ambalo lilikuwa likiinga Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii. 



Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, linawashikilia watu zaidi ya 200 kwa tuhuma mbalimbali likiwemo kwa watu Raia wa China kutapeliwa dola za kimarekani 800 kwa kutumia jina la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. 

Akizungumza na waandishi wa habari , Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro amesema kukamatwa kwa watu hao imetokana na operesheni zinazoendelea katika jiji la Dar es Salaam kuhakikisha wananchi na mali zao wanaishi kwa amani. 

Amesema katika waliokamatwa ni pamoja ni panya road saba waliomvamia Nyumbani kwa Askari wa Jeshi la Wananchi , Ladislaus Kaitaba. 

Katika tukio waliweza kukamata mtandao wa panya road kwa kutumia Ramadhani Ndabi (35)ambaye alichukua simu ya askari hiyo baada ya kupiga akapatikana na kuanza kutaja wenzie wanaofanya matukio. 

Aidha amesema kuwa wizi wa magari unaendelea lakini polisi waliweza kukamata gari lilokuwa likiuzwa kwa kujifanya wateja na ilipogundulika walioiba wakatoweka. 

Kamanda Sirro amesema kuwa bangi imekuwa ikiingzwa kwa njia nyingi na sasa watu wanatumia mabegi wakiwa wasafiri kumbe wanakuwa wameweka bangi.

No comments: