Sunday, October 23, 2016

MFALME MOHAMED VI KUTOKA TAIFA LA MOROCCO AWASILI JIJINI DAR JIONI HII, APOKELEWA NA MWENYEJI WAKE RAIS DKT MAGUFULI

Pichani ndege aina ya Boeing 747 iliyombeba Mfalme Mohamed VI wa Morocco na ujumbe wake ikiwasili katika uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere,jioni hii jijini Dar na kulakiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.
Pichani ndege aina ya Boeing 747 iliyombeba Mfalme Mohamed VI wa Morocco na ujumbe wake ikiwasili katika uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere,jioni hii jijini Dar na kulakiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli akiwa na Mgeni wake,Mfalme Mohamed VI kutoka taifa la Morocco wakipata Gwaride la heshima,mara baada ya kuwasili Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar jioni hii.Mfalme huyo amewasili jioni ya leo kwa ziara ya kikazi ya siku tatu,aidha imeelezwa kuwa Mfalme huyo aliyekuja na ujumbe wa watu takribani 1000,mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku tatu,atakuwa na siku nyingine tano za mapumziko hapa nchini ambapo atatembelea maeneo mbalimbali ya vivutio na utalii nchini Tanzania
Sehemu ya ujumbe alioongozana nae Mfalme Mohamed VI kutoka Taifa la Morocco,aliyewasili jioni ya leo na kulakiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli 

No comments: