Saturday, October 01, 2016

KATIBU MKUU WA CCM, KINANA AKUTANA NA KATIBU MKUU WA CHAMA CHA CNDD-FDD CHA BURUNDI, JIJINI DAR ES SALAAM, LEO


 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake, akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa chama cha CNDD-FDD Evariste Ndayishimiye na ujumbe wake, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
Kataibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimkaribisha Katibu Mkuu wa Chama cha CNDD-FDD, Evariste Ndayishimiye, leo Oktoba 1, 2016, katika Ofis Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kuwa na mazungumzo baina ya viongozi hao kuhusu uhusiano wa vyama hivyo ya CCM na CNDD-FDD. Kushoto ni Mnadhimu Mkuu wa CNDD-FDD, Gelase Ndabirabe.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Katibu Mkuu wa Chama cha CNDD-FD cha Burundi wakifurahia jambo wakati wa mazungumzo yao katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo.
 Baadhi ya maofisa katika ujumbe wa Burundi uliofuatana na Katibu Mkuu wa Chama cha  CNDD-FDD Evariste Ndayishimiye, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam

No comments: