Wednesday, January 22, 2014

MAMIA WASHIRIKI MAZISHI YA MAMA MZAZI WA ALIYEKUA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM NA KATIBU MKUU WA CCM MZEE YUSUF MAKAMBA

 Mzee Yusufu Makamba akishauriana jambo na mwanae January Makamba wkati wa shughuli za mazishi zikiendelea.Mzee Yusufu Makamba amefiwa na mama yake mzazi aliyefahamika kama Mariam Masau Kivugo  kilichotokea tarehe 21 January 2014.
 Mzee Yusufu Makamba akiwa na mwanae January Makamba wakitafakari jambo baada ya kupata msiba mkubwa  wa kufiwa na Mama mzazi wa Mzee Yusufu Makamba, Mariam Kivugo.
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ndugu Abdallah Majura Bulembo akitoa salaam za pole kwa wafiwa wakati wa mazishi ya Bibi Mariam Masau Kivugo.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa salaam za pole kwa niaba ya Chama  kwa Mzee Yusufu Makamba na Familia yake wakati wa mazishi ya Mama wa Mzee Yusufu Makamba.
 Mamia ya watu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Ndugu January Makamba wakati akitoa salaama za shukrani kwa niaba ya familia kwa wananchi wote waliojitokeza kwenye mazishi ya Bibi yake Marehemu Mariam Masau Kivugo yaliyofanyika Mehazangulu, Tanga.
 Mwili wa Marehemu Mariam Kivugo ukipelekwa msikitini kwa ajili ya kuombewa kabla ya kuelekea makaburini.
 Watu wakiwa kwenye nyuso za huzuni wakati wa mazishi ya Bibi Mariam Kivugo ambaye pia ni mama wa Mzee Yusufu Makamba.
Katibu wa NEC itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki kuweka udongo kwenye kaburi la mama wa Mzee Yusuf Makamba aliyefariki tarehe 20 Januari 2014.Picha Zote na Adam Mzee

No comments: