Friday, January 17, 2014

SHIRIKA LA NYUMBA NHC LATOA MAFUNZO KWA VIKUNDI VYA VIJANA 50 WA NCHI NZIMA

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, (NHC) Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na waandishi wa habari. Shirika la Nyumba la Taifa kwa kushirikiana na Wakala wa Utafiti wa Vifaa Bora vya Ujenzi (NHBRA) iliyo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, pamoja na VETA mmetoa mafunzo kwa wataalam wapatao 50, wawili kutoka  kila Mkoa ambao baadae watatumika kutoa mafunzo kwa vijana katika  Halmashauri za Wilaya na Miji kuanzia mwezi Januari hadi Juni 2014.  Mafunzo hayo yanahusu namna ya kutumia mashine hizo na kutambua udongo unaofaa kutengenezea matofali na namna ya kujenga kutumia hayo matofali. 
Washiriki wa mafunzo wakiwa katika eneo la mradi Chamazi, Dar es Salaam, Mradi huu ni mali ya wapangaji walioondolewa katika bomoa bomoa ya utanuzi wa Bandari eneo la Keko na Kigamboni wakaamua kuunda umoja wa wamiliki wa nyumba za gharama nafuu eneo la Chamazi ukiitwa Federation.
1Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akizungumza wakati wa maandalizi ya ufungaji wa mafunzo ya vijana wawakilishi wa vikundi  kutoka mikoa mbalimbali kuhusu utengenezaji wa matofali ya ya udongo yenye teknolojia ya Interlocking Blocks yaliyoanza Januari 6 mpaka 17 mwaka huu ambayo yanatarajiwa kufungwa wiki ijayo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda, Mkurugenzi huyo amesema Shirika la nyumba badala ya kwenda kutoa msaada wa sabuni na vyakula katika vituo vya watoto yatima au kusaidia biskuti limeamua kubadilisha maisha ya vijana wa Tanzania kwa kuwapa mafunzo  na kuwapatia mashine za kutengeneza matofali ya udongo ambayo wao NHC watakuwa ndiyo wateja wakuu wa kununa matofali hayo, lakini pia shirika hilo linatoa mashine za kufyatulia matofali  zipatazo 640 katika wilaya 160 mikoa yote ya Tanzania bara na kiasi cha shilingi 500,000 kila mkoa  kama mtaji wa kununulia saruji kwa vikundi hivyo, Katikati ni Dk Simioni Kintingu Mkurugenzi Mkuu wa  National Housing & Building Research Agency (NHBRA) na kushoto ni Bw. Julius Mjelwa kutoka VETA, mafunzo hayo yameratibiwa kwa pamoja na (NHC), (VETA) na (NHBRA) kwa pamoja.

2Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akizungumza akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari leo.3Dk Simioni Kintingu Mkurugenzi Mkuu wa  National Housing & Building Research Agency (NHBRA) akifafanua masuala ya kitaalamu kuhusu teknolojia hiyo ya matofali kwa waandishi wa habari.4Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo.5Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo.7Baadhi ya maofisa wa Shirika la Nyumba NHC wakiwa katika maadalizi hayo kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Jamii, Susan Omary Meneja Mawasiliano NHC, Muungano Saguya Meneja huduma kwa jamii NHC na Ephraim Kibonde mtangazaji wa Clouds Radio.

No comments: