Thursday, January 02, 2014

IGP ERNEST MANGU, NAIBU WAKE WAAPISHWA NA JK, DAR



Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Mkuu mpya wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Ernest Mangu, kwenye hafla iliyofanyika viwanja vya Ikulu, Jumanne jioni Disemba 31, 2013. Rais pia alimuapisha naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi (D-IGP), Abdulrahman O.J.Kaniki. nafasi hiyo ya D-IGP ni mpya. Katika hafla hiyo, Makamu wa rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, waziri wa nchi ofisi ya rais (Uratibu na Mahusiano ya Jamii), Steven Wasira, waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu (Bunge na Uratib), William Lukuvi, Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba, Mathias Chikawe na Naibu waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Silima walihudhuria. Halikadhalika wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, walikuwepo bila kuwasahau maafisa wote wa vyeo vya juu wa jeshi la polisi nao walihudhuria sherehe hiyo

D-IGP Kaniki alika kiapo mbele ya Amiri Jeshi Mkuu, Rais Kikwete

Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete, akiwasili eneo la tukio, Ikulu

Huyu ndiyo Ernest Mangu, IGP mpya

Huyu ndiyo Abdulrahman O.J Kaniki (D-IGP), mpya. Kaniki anakuwa mtanzania wa kwanza kushika cheo hicho kipya

D-IGP, Kaniki akifunga kamba za viatu kabla ya kuanza kwa kiapo

Rais Kikwete, makamu wa rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, IGP mpya Ernest Mangu (Watatu kulia) D-IGP Abdulrahman O.J.Kaniki (Kulia) na IGP aliyemaliza muda wake, Said Mwema (Kushoto)

JK akifanya mzaha na IGP wake Mangu

JK na familia ya Mangu

JK na familia ya Kaniki

JK na familia ya Mwema

JK na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama

IGP Mangu (Kulia) na D-IGP Kaniki

IGP Mangu akijibu maswali ya waandishi mara baada ya kuapa kushika wadhifa huo

JK akimpongeza D-IGP, Kaniki

JK akimkabidhi muongozo D-IGP, Kaniki

JK akipokea saluti kutoka kwa IGP Mangu

JK akimpongeza IGP Mangu

IGP Mangu akipokea kadi ya kumtakia heri kutoka kwa mtangulizi wake, Said Mwema

D-IGP, Kaniki, akipokea kadi ya kumtakia heri kutoka kwa bosi wake wa zamani IGP mstaafu Mwema, huku mama Mwema kulia na IGP mpya Mangu wakishuhudia

IGP Mangu akipokea shada la maua kutoka kwa mkewe wakati wa pongezi baada ya kula kiapo cha kushika wadhifa huo

No comments: