Friday, January 24, 2014

DK MAGUFULI AHAMIA MOROGORO KUSIMAMIA UJENZI DARAJA LA DUMILA LILILOSOMBWA NA MAJI


Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli akiwa katika gari linaloendelea na ujenzi wa daraja la Dumila.
Waziri Magufuli akitoa maelekezo kwa watendaji wa Tanroads.…
Waziri Magufuli akitoa maelekezo kwa watendaji wa Tanroads.
Sehemu ya barabara iliyozolewa na maji ya mto Mkundi.
Waziri wa Ujenzi akikagua maeneo yaliyoharibika.
Dk. Magufuli akiendelea na kazi katika daraja hilo.
Kazi za ujenzi zikiendelea eneo hilo la daraja lililoharibika.
Dk. Magufuli akiwapa hi mafundi wanaoendelea na ujenzi wa daraja hilo
WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli amepiga kambi mkoani Morogoro kusimamia mwenyewe ujenzi wa Daraja la Dumila ambalo ni kiungo muhimu cha barabara ya Dodoma – Morogoro lililosombwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia tarehe 22.01.2014 na kusababisha magari kutopita kabisa ama yanayotoka upande wa Dodoma au Morogoro. Mbaya zaidi hakuna njia nyingine mbadala zaidi ya hiyo.

No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...