Monday, January 27, 2014

Uzinduzi wa Operesheni M4C Pamoja Daima Mbeya,Kigoma Kaskazini Mkongoro,Njombe,Bukoba,Chimala, Mbarali,Mwanga Kigoma,Ngara,Singida


 Mbunge wa singida magharibi tundu lissu akizindua Operesheni M4C Pamoja Daima singida 
  Umati wa watu ikishangilia  ukishuhudia wakati helcopter ikitua bukoba na mwenyekiti wa chadema na mbunge wa hai freeman mbowe alipotua kuzindua operesheni M4C pamoja daima
Mwenyekiti wa chadema na mbunge wa hai freeman mbowe akimvisha rasmi bendera ya chadema mmoja kati ya wafuasi wa ccm waliojiunga na chadema bukoba
 Katibu mkuu wa chadema Dr Wilbrod Slaa akijianda kutua na helikopta ya chadema mkoani mbeya jana
  Katibu mkuu wa chadema Dr Wilbrod Slaa akijianda kutua na helikopta ya chadema makambako  pamoja na mvua kubwa iliyokua ikinyesha wananchi wa makambako walijitokeza kwa wingi sana, kumsikiliza katibu mkuu wa chadema dr slaa
  Katibu mkuu wa chadema Dr Wilbrod Slaa(kulia kwenye jukwaa) akihutubia mamia ya wapenzi na wanachama wa chadema chimala muda mfupi baada ya  kutua na helikopta ya chadema   pamoja na mvua kubwa iliyokua ikinyesha wananchi wa makambako walijitokeza kwa wingi sana, kumsikiliza katibu mkuu wa chadema dr slaa
   Katibu mkuu wa chadema Dr Wilbrod Slaa akihutubia mami ya wapenzi na wanachama wa chadema makambako muda mfupi baada ya  kutua na helikopta ya chadema   pamoja na mvua kubwa iliyokua ikinyesha wananchi wa makambako walijitokeza kwa wingi sana, kumsikiliza katibu mkuu wa chadema dr slaa
 Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Mendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa akiwasili katika mji wa Chimara mkoani Mbeya, ambako alifanya mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika jana.
 Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, akihutubia mkutano wa hadhara ikiwa ni mfululizo wa mikutano ya Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika katika mji wa Chamara mkoani Mbeya jana.
 Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa akiwahutubia wananchi wa mji wa Makmabako, katika mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika jana.
 Wananchi wa mji wa Njombe na vitongoji wakiwa katika mkutano wa hadhara wa Operesehni M4C Pamoja Daima, wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), uliofanyika mjini Njombe jana.
 Aliyekuwa Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tawi la Isitu, Chimara mkoani Mbeya, Felix Komba akizungumza katika mkutano wa Operesehni M4C Pamoja Daima mbele ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, baada ya katibu huyo kujiunga na Chadema wakati wa mkutano huo uliofanyika Chimara jana
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Cadema), Dk. Willibrod Slaa akimnadi mgombea udiwani katika Kata ya Njombe Mjini kupitia chama hicho, Agrey Mtamba, wakati wa mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika mjini Njombe jana.
 Baadhi ya wananchi wa mji wa Mbeya wakiwa wabeba mabango yenye ujumbe mbalimbali, wakati wa mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C Pamoja Daima wa Chadema, uliofanyika kwenye Uwanja wa Lwanda Nzovwe mjini Mbeya jana
 Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, akiwahutubia wananchi wa mji wa Mbeya na vitongiji vyake katika mkutano wa hadhara wa Operesehni M4C Pamoja Daima, uliofanyika kwenye Uwanja wa Rwanda Nzovwe jana.
 Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa akihutubia mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika kwenye Uwanja wa Rwanda Nzovwe jana.
  Mbunge wa Mbozi Mashariki, Davi Silinde (Chadema), akiwahutubia wananchi wa mji wa Mbeya, katika mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C Pamoja Daima uliofanyika kwenye Uwanja wa Rwanda Nzovwe mjini Mbeya jana.
 Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa akiwa amembeba mtoto Sheila Shukurani (3), kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara matika mji wa Makongorosi mkoani Mbeya jana.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, wakiondoka kwa shamrashamra, baada ya kuhutubia mkutano wa hadahara wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika katika mji wa Makongorosi mkoani Mbeya jana.
  Mbunge wa Singida Magharibi Tundu Lissu akizindua Operesheni M4C Pamoja Daima Singida
Mbunge wa Singida Magharibi akihutubia mamia ya wanachama wa Chadema karatu wakati wa uzinduzi wa operesheni pamoja daima 
Mbunge wa arumeru mashariki joshua nassari akihutumia mamia ya wapenzi wa chadema wakati wa uzinduzi wa operesheni pamoja daima ya Chadema  Ngarenanyuki Arumeru Mashariki
M/Kiti wa Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) Mh. John Heche akiunguruma kwenye uzunduzi wa operesheni pamoja daima ya chadema  Ngarenanyuki Arumeru Mashariki mbele ya mamia wa wanachama
Mbunge Singida Magharibi Tundu Lissu akipokea kadi za wanachama wa CCM waliyoamua kujiunga na Chadema rasmi wakati wa uzinduzi wa operesheni pamoja daima Iramba Singida 
 Mbunge wa Ubungo-John Mnyika (kushoto) na Mbunge wa arusha Godbless Lema (katikati) wakipungia wananchi na wapenzi wa chadema muda mfupi baada ya kutua kigoma kaskazini Mkongoro
 Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai akipokea kadi mbalimbali  kutoka kwa wanachama wa CCM waliamua kujiunga na chadema rasmi
  Mbunge wa ubungo john mnyika akihutubia mamia ya wanapenzi na wanachama wa chadema wakati wa uzinduzi wa operesheni pamoja daima 
 Makamu mwenyekiti wa Chadema  Zanzibar Said Issa Mohamed akiwa ndani ya chopa ya chadema muda mfupi kabla ya kutua bukoba kuzindua operesheni M4C pamoja Daima
 Mbunge wa Arusha mjini (kulia) Godbless Lema na Mbunge wa Ubungo John Mnyika wakiwa kwenye chopa helikopta ya chadema wakielekea kwenye uzinduzi wa Operesheni M4C Pamoja Daima Kilelema
 Viongozi wa chadema wakiwa Kigoma Kaskazini Mkongoro muda mfupi baada ya kutua na chopa kuzindua operesheni pamoja daima. Picha Zote na Chadema

No comments: