Wednesday, November 18, 2009

Mama Kikwete ziarani Singida


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) akiwa amebeba kibuyu mara baada ya kukabidhiwa na wanawake wa kabila la wataturu ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika mkoa wa Singida. Mama Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo.Picha na Juma Kengele - Ikulu

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) akisalimiana na mtoto Neema Jackson mwenye umri wa miaka miwili wakati alipotembelea Hospitali ya wilaya ya Manyoni kwa ajili ya kufungua wodi ya watoto.

SERIKALI YAZITAKA TAASISI ZOTE KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

  Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. James Kilabuko. Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti...