KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-Moon atatembelea Tanzania baadaye mwezi huu, imethibitishwa mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Ban Ki-Moon amethibtisha mwenyewe kuhusu ziara hiyo ya siku mbili, kuanzia Februari 25, mwaka huu.
Katibu Mkuu huyo alitangaza ziara hiyo wakati alipokutana na kuzungumza na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, katika Kituo cha Mikutano cha UNCC-ECA mjini Addis Ababa.
Viongozi hao wawili wako mjini Addis Ababa, Ethiopia, kuhudhuria mkutano wa 12 wa kawaida wa viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU).
Ban Ki-Moon alisema atazuru Tanzania baada ya kumaliza ziara yake nchini Afrika Kusini.
Hii itakuwa ziara ya kwanza kwa Katibu mkuu huyo wa UN, kutembelea Tanzania.
Katika mazungumzo hayo, Ki-Moon, alimsifia Naibu Katibu Mkuu wa UN, Dk Asha Rose Migiro wa Tanzania, kwa kuwa mwanamke mchapa kazi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA AMALIZA ZIARA YA SIKU MOJA MKOANI MBEYA
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), leo ameondoka Mkoani Mbeya baada ya kukamilisha zi...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
No comments:
Post a Comment