Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Rais Jakaya Kikwete amemvua madaraka na kumwachisha kazi rasmi kuanzia jana mkuu wa wilaya ya Bukoba, Albert Mnali aliyeamuru polisi mmoja kuwachapa viboko walimu katika shule tatu za msingi zilizo wilayani kwake kutokana na kushika mkia katika matokeo ya darasa la saba.
Taarifa iliyotolewa na ofisi ya Waziri Mkuu jana ilieleza kuwa Rais Kikwete amechukua hatua hiyo ili iwe fundisho kwa kuwa kitendo alichokifanya Mkuu huyo wa wilaya hakikubaliki, kimedhalilisha, cha kuvunja moyo walimu na kinavunja maadili ya kibinadamu.
Katika uamuzi huo, Rais Kikwete alisema mkuu huyo wa wilaya amedhalilisha wadhifa wa ukuu wa wilaya kwa kuwa alikosea kuchukua hatua hiyo kwa kuwa mwenye mamlaka ya kuwawajibisha walimu ni kamati za nidhamu za mikoa na wilaya na wala si mtu mmoja kama alivyofanya mkuu huyo.
Alisema kuwa amechukua hatua hiyo baada ya kufuatilia maelezo ya pande zote zinazohusika na kuwa serikali imeridhia kiongozi huyo avuliwe wadhifa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
TANZANIA NA COMORO ZAENDELEZA USHIRIKIANO WA KISWAHILI KWA KUANZISHA MAZUNGUMZO YA KUFUNDISHA LUGHA HIYO MASHULENI
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, kupitia kwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Victoria Mwanziva, ametamka kuwa Serikali inatambua na ...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
No comments:
Post a Comment