*Ni kwa matokeo mabaya darasa la saba
*Waziri asema katu hawawezi kuvumilia
MKUU wa wilaya ya Bukoba Albert Mnali, amemwamuru askari polisi mmoja kuwapiga viboko walimu katika shule tatu za msingi zilizoko Wilaya ya Bukoba kwa sababu wilaya hiyo imekua ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba.
Tukio hilo lilitokea juzi wakati mkuu huyo wa wilaya Koplo wa polisi aliyeambatana naye kwa kuwalaza chini walimu hao na kumuamuru koplo huyo kuwadhibu viboko viwili makalioni na mikononi.
Walimu waliocharazwa viboko tisa wanatoka shule ya msingi Katerero, 11 wa shule ya msingi Kanazi ambao walichapwa viboko viwiwili kila mmoja na walimu 12 kutoka shule ya msingi Kansenene viboko vinne vinne kila mmoja.
Akizungumza jana waandishi wa habari juu ya tukio hilo mkuu huyo wa Wilaya alisema alilazimika kuwatandika viboko walimu hao baada ya kugunda au kuwepo uzembe kazini, ikiwemo kuchelewa kufika kazini na kutofundisha kama mikataba yao ya ajira inavyosema. Taarifa zaidi punde
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
TANZANIA NA COMORO ZAENDELEZA USHIRIKIANO WA KISWAHILI KWA KUANZISHA MAZUNGUMZO YA KUFUNDISHA LUGHA HIYO MASHULENI
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, kupitia kwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Victoria Mwanziva, ametamka kuwa Serikali inatambua na ...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
No comments:
Post a Comment