Tuesday, July 15, 2025

RAIS MWINYI AWASILI JIJINI ARUSHA






Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewasili Jijini Arusha leo kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Mabaraza Huru ya Habari Afrika, unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha – AICC.

Mheshimiwa Rais Mwinyi ameondoka Zanzibar mapema leo na kuwasili salama katika Uwanja wa Ndege wa Arusha, ambako amepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Kenani Laban Kihongosi, pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali, na maafisa kutoka vyombo vya ulinzi na usalama wa mkoa huo.

Mkutano huo wa Afrika unalenga kujadili nafasi ya vyombo huru vya habari katika kukuza demokrasia, uwajibikaji na utawala bora barani Afrika.

No comments:

WIZARA YA AFYA YAOMBA SH. TRILIONI 1.8 BAJETI YA 2026/2027

  Wizara ya Afya imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma z...