Sunday, July 06, 2025

🌍 KIKUNDI CHA JWTZ CHATINGISHA COMORO KWA KWATA YA KIMYA KIMYA!

 






Moroni, Comoro – Julai 6, 2025

Kwa ustadi wa hali ya juu, kikundi maalum cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kimeonesha umahiri wa kupiga kwata ya kimya kimya wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Comoro yaliyofanyika tarehe 6 Julai 2025, katika Uwanja wa Malouzini, Moroni.

Uhodari na nidhamu ya askari wa JWTZ vimeacha gumzo na kuwavutia maelfu ya watazamaji waliokuwepo kushuhudia tukio hilo la kihistoria. Hii ni ishara ya mshikamano wa kweli, urafiki wa muda mrefu, na heshima ya Tanzania kwa nchi marafiki kama Comoro.

Akizungumzia tukio hilo, mmoja wa viongozi wa majeshi ya ulinzi wa Comoro alieleza kuwa Tanzania ni ndugu wa kweli wa kihistoria kwa Comoro, si tu kwa msaada wa ukombozi, bali pia kwa namna inavyoendeleza uhusiano wa kijeshi na kijamii.

Ushiriki wa JWTZ katika maadhimisho haya ni ishara ya msimamo wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wa kuimarisha mahusiano ya kimataifa kupitia diplomasia ya kijeshi, mshikamano wa kanda, na utangamano wa Afrika.

@Beit_Salam @PresidenceUnionComores #JWTZ #KwataKimyaKimya #UhuruComoro50 #TanzaniaComoro #DiplomasiaYaKijeshi #AfricaUnited

No comments:

DKT. MWIGULU AWASILI SONGEA KUSHIRIKI IBADA YA KUAGA MWILI WA JENISTA MHAGAMA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Desemba 15, 2025 amewasili mjini Songea mkoani Ruvuma kwa ajili ya...