Thursday, November 15, 2007

Richard ndani ya Bongo





Mshindi wa Big Brother II Africa Richard akiwa katika kikao cha waandishi wa habari kilichofanyika katika hoteli ya Holiday Inn iliyopo maeneo ya Posta Jijini Dar es Salaam leo, kulia ni meneja wa Multichoice hapa nchini (Lucy Kihwele) na kushoto ni mmoja wa maafisa wa Multi choice aliyefahamika kwa jina la Shelukindo.


Baba mzazi wa Richard Bezuidenhout naye alikuwepo katika uwanja wa Ndege wa Jk Nyerere Jijini Dar es Salaam wakati wakimpokea mwanae baada ya kushinda Big Brother Africa II.




Ndugu wa Richard,Louis naye alikuwa ni miongoni mwa Watanzania waliofurika kumpokea Mshindi huyo.





Ama kweli Richard ameleta mambo Mabaunsa , familia baba, kaka na dada zake , wabongo kibao walijaaa uwanjani hapo kuhakikisha usalama wa kutosha unapatikana na baadaye leo kazungumza na vyombo vya habari. Picha za Richard Bukos wa Global Publisherz na Mpoki Bukuku.

No comments: