RAIS Jakaya Kikwete ameteua wajumbe wa Kamati ya uangaliaji upya mikataba ya uchimbaji wa madini nchini itakayo kuwa na jukumu la kupitia mikataba ya madini na nyaraka nyingine zitakazohusu migodi ya mikubwa nchini.
Kamati hiyo yenye jumla ya wajumbe kumi na mmoja itakuwa chini ya Uenyekiti wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali mstaafu, Jaji Mark Bomani.
Wengine ni pamoja na:-
Zitto Kabwe- Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA),
John Cheyo -Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP),
Salome Makange- Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini
Mugisha Kamugisha- Kamishina wa Sera Wizara ya Fedha
Edward Kihundwa- Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi
Dk. Harrison Mwakyembe- Mbunge wa Kyela (CCM)
Ezekiel Maige- Mbunge wa Msalala (CCM)
Peter Machunde- Soko la Hisa, Dar es Salaam (DSE)
David Tarimo- Mkaguzi wa Mahesabu kutoka Shirika la Kimataifa la CoopersHouse
Maria Kejo- Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa, Wizara ya Katiba na Sheria
Taarifa ya Ikulu iliyosainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi ilisema kuwa pamoja na mambo mengine kamati hiyo pia itakuwa na kazi ya kuchambua mfumo wa kodi unaotumika katika sekta ya madini na kupitia mfumo wa usimamizi wa shughuli za uchimbaji mkubwa unaofanywa na serikali.
Kamati hiyo iliyopewa kipindi cha miezi mitatu kukamilisha kazi yake pia inajukumu la kukutana na chamber of minerals na wadau wengine na kutakiwa kutoa taarifa yenye mapendekezo.
Kuundwa kwa Kamati hiyo kunafuatia hoja binafsi ya mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe aliyoitoa bungeni kutaka kuundwa kwa kamati itakayochunguza mikataba ya madini kufutia Waziri wa Nishati, Nazir Karamagi kutia saini makubalino ya uchimbaji wa madini katika mgodi wa Buzwagi akiwa nje ya nchi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA AMALIZA ZIARA YA SIKU MOJA MKOANI MBEYA
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), leo ameondoka Mkoani Mbeya baada ya kukamilisha zi...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
No comments:
Post a Comment