Rais Jakaya Mrisho Kikwete alikagua barabara ya Lindi – Kibiti hadi Mingoyo pamoja na Daraja la Mbwemkuru, wakati akitoka Lindi kwenda Kilwa.
Kabla ya ukaguzi huo, Rais alipata taarifa ya maendeleo ya barabara hii muhimu kwa mikoa ya kusini na Daraja la Umoja (ambalo hakulikagua) kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Bw. Omar A. Chambo; ambaye amemueleza Rais kuhusu hatua mbalimbali zilizofikiwa katika ujenzi wa barabara hiyo. Ujenzi wa barabara ambao unafanyika kwa awamu, utakamilika mwishoni mwa mwaka huu wakati Daraja la Umoja linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2008.
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari Msaidizi wa Rais,
20 Nov, 07.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
WAZIRI MKUU: SERIKALI YAENDELEA KUHAKIKISHA MAFUTA HAYAADIMIKI NCHINI
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini unaendelea ...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Pascal Mayalla akiwa katika chumba cha wagonjwa Daraja la kwanza katika hospitali ya mkoa wa Dodoma ambako amelazwa kwa matibabu baada ya ku...
No comments:
Post a Comment