Monday, November 05, 2007

Matokeo taratibu tartibuu

picha kutoka kwa mdau MPOKI ana picha nyingi huyo na kiboko zaidi.

MATOKEO ya uchaguzi wa nviongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) yametoka na sasa watu wanashangilia na wengine kufuta machozi hebu cheki hawa. Wanalia.

Katika nafasi za kundi la wanawake Tanzania Bara kuna
Mbunge wa zamani wa Afrika Mashariki na sasa Mbunge Beatrice
Shelukindo. Pia yupo Mbunge Tatu Ntimizi na Katibu Mkuu mstaaf wa
UWT Halima Mamuya.

Kwenye kundi la Vijana kuna wagombea Hussein Mohamed ambaye
alionekana kufanya kampeni maeneo mengi ya nchi na kuonyesha kuwa
angeibuka mshindi naKiongozi katika ofisi ya UVCCM taifa, Fransis
Issack walitupwa.

Kwa upande wa Issack, hili ni pigo lingine kufuatia kupoteza nafasi zote
alizogombea mkoani Singida huku akitajwa kuwa na nia ya kusaka kiti cha
Mwenyekiti wa UVCCM ngazi ya taifa katika uchaguzi utakaofanyika mwakani.

Danhi Makanga, Ruth Msafiri, Thomas Ngawaiya na Tambwe Hiza wamepoteza katika kundi hili. Ngawaiya na Hiza
walitoka upinzani na walitarajiwa kupewa kura za huruma jambo ambalo
halikufanyika.

Wengine nni pamoja na wabunge Margareth Agness Mkanga, Zuhura Mikidadi na mhamasishaji wa tenzi wa CCM, Salim Shomvi Tambalizeni, Naibu Meya wa Ilala Mustafa Yakub, Mkuu wa Mkoa wa Mara Isdore Shirima na Mkuu wa Wilaya ya
Frank Uhaula walikosa nafasi hizo.

Wanasiasa wengine maarufu waliokosa nafasi baada ya kupata kura chache ni Wilson Masilingi, Brigedia Jenerali Mstaafu Hassan Ngwilizi, Tarimba Abbas, Filbert Bayi, Enock Chambiri, Christopher Gachuma, Charles Kagonji, Lukas Kisasa, Pascal Mabiti, Dk James Msekela, Profesa Idrisa Mtulia, Abeid Mwinyimsa na Job Ndugai.

Wengine ni wandishi wa habari Jacqueline Liana, Jeni Mihanji na Novatus Makunga.

Hawa mambo yao supa toka katika kundi gumu lenye wagombea 59 washindi ambao ni 20 ni wafuatao!
Edward Lowassa, Andrew Chenge, Yusufu Makamba, Bernard Camilius Membe, Jaka Mwambi, Juma Otman Kapuya, Abrahman Kinana, Christopher Gachuma, Stephen Masatu Wassira, Aggrey Mwanri, Milton Makongo Mahanga, Fredrick Tluway Sumaye, John Komba, Kingunge Ngombale Mwiru, William Lukuvi, John Chiligati, Amos Makalla, Samwel Wangwe, David Homeli Mwakyusa na Jackson Msome

No comments: