Na Nora Damian wa Mwananchi
UBISHI makali ulizuka katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam jana wakati wa mahojiano kati ya Wakili Gabriel Mnyele kwa upande wa wadaiwa na shahidi wa pili Daudi Kamugisha (40) kwa upande wa wadai katika kesi ya madai ya kashfa ya inayosikilizwa na Jaji Augustino Shangwa.
Katika kesi hiyo, wadai ni waumini wa dhehebu la Katoliki wa Shirika la Ndugu Wadogo wa Afrika, wanaopinga habari iliyoandikwa Mei 29 mwaka 2005 katika gazeti la Majira zikidai kuwa wafuasi wa shirika hilo wanalazimisha kuwinda na kula nyama ya nyoka na kutembea pekupeku.
Kwa mujibu wa kesi hiyo, anayayedaiwa kuwashurutisha wafuasi hao ni mwanzilishi wa shirika hilo, Padre Riccarido Enrico, mwenye asili ya Italia ambaye sasa ni raia wa Tanzania na amekuwepo nchini kwa zaidi ya miaka 20 akitoa bure huduma za elimu ya sekondari mbali na huduma za kiroho. Soma MWANANCHI kwa taarifa zaidi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS SAMlA AFANYA MAZUNGUMZO NA MJUMBE MAALUM WA RAIS TSHISEKEDI
Dar es Salaam, 26 Machi 2025 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan , amekutana na kufanya mazungu...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Kwa wale waliokulia maeneo haya, hili ni jambo la kawaida ukitoka mjini, shambani sijui hadi wapi kote ni haya h...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment