Thursday, July 31, 2025

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI KUZINDUA BANDARI KAVU YA KWALA – PWANI












Pwani, Julai 31, 2025 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo ameweka jiwe la msingi kuashiria uzinduzi rasmi wa Bandari Kavu ya Kwala, iliyopo katika Mkoa wa Pwani, hatua muhimu katika kuimarisha miundombinu ya usafirishaji na uchumi wa taifa.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na viongozi wa Serikali, wadau wa sekta ya usafirishaji na wananchi wa mkoa wa Pwani, Rais Samia ameeleza kuwa mradi huu ni sehemu ya mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za bandari, kupunguza msongamano katika Bandari ya Dar es Salaam, pamoja na kuchochea maendeleo ya viwanda na biashara ndani na nje ya nchi.

“Bandari Kavu ya Kwala ni nyongeza muhimu kwa mfumo wa kitaifa wa usafirishaji mizigo. Kupitia mradi huu, tunatarajia kuongeza kasi ya ushindani wa bandari zetu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati, huku tukifungua fursa zaidi za ajira, biashara na uwekezaji,” alisema Rais Samia.

Bandari hiyo imejengwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi, ikiwa na uwezo wa kuhudumia makasha zaidi ya 500,000 kwa mwaka. Pia ina miundombinu ya kisasa ikiwemo maghala, njia za reli na barabara zinazounganisha moja kwa moja na Bandari ya Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, amesema kuwa Bandari Kavu ya Kwala itapunguza muda wa utoaji wa mizigo kutoka siku kadhaa hadi masaa machache, hivyo kuongeza tija katika shughuli za kiuchumi.

Uzinduzi wa bandari hii unatazamwa kama ushahidi wa dhamira ya Serikali kuendelea kuwekeza katika miradi mikubwa ya kimkakati kwa ajili ya kukuza uchumi wa taifa, kuimarisha huduma za usafirishaji, na kujenga Tanzania ya viwanda.

#BandariKavuYaKwala
#MiundombinuBora
#SamiaSuluhuHassan
#TanzaniaInajengwa
#UchumiWaBuluu
#Pwani2025

Fuatilia mitandao yetu ya kijamii 

Instagram: @mamakajatz

Twitter @mamakajatz

Facebook: Mamakajatz

YouTube: Mama kaja tz 

#Mamakaja #kaziiendelee

NCAA YANOGESHA “WORLD RANGERS DAY” KWA KUFANYA MICHEZO NA SHUGHULI ZA KIJAMII KARATU






Na Philomena Mbirika, Karatu Arusha.

Mamlaka ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) imehitimisha maadhimisho ya siku ya askari Wanyamapori duniani kwa kufanya michezo mbalimbali iliyohususu askari wa Jeshi la Uhifadhi, askari wa Jeshi la polisi wilaya ya Karatu pamoja na kufanya shughuli ya upandaji miti katika shule ya Sekondari Welwel iliyopo Karatu Mkoani Arusha.

Kamishna wa Uhifadhi NCAA ameongoza maafisa na askari katika zoezi la kupanda miti Shule ya Sekondari Welweli, kutoa elimu ya shughuli za uhifadhi na utunzaji wa mazingira kwa wanananchi na kuongoza watumishi hao katika michezo mbalimbali ikiwemo kukimbia kilomita tano, mchezo wa mpira wa miguu kati ya askari wa jeshi la Uhifadhi kutoka pori lla akiba Pololeti, askari walioko eneo la hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Polisi Karatu.

“NCAA ni sehemu ya Jamii, katika utekelezaji wa majukumu yetu tunashirikiana na vyombo vingine ikiwepo Polisi Wilaya za Ngorongoro na karatu pamoja na wananchi, ndio maana leo tumefanya michezo ya riadha, mazoezi yaa viungo, mchezo wa mpira wa miguu ili kuendelea kutuweka pamoja hasa katika shughuli za kuimarisha usalama na ulinzi wa rasilimali za Nchi) alifafanua Kamaishna Badru.

Badru ameeleza kuwa NCAA pia ina jukumu la kutoa elimu ya mazingira na uhifadhi shirikishi kwa jamii zinazozunguka hifadhi ya Ngorongoro, hivyo katika kuadhimisha siku ya askari wa Wanyamapori imetoaa miti bure kwa wananchi ili wakapande katika maeneo yao na kupanda miti katika shule ya Sekondari Welwel kisha kuzungumza na walimu na wanafunzi wa shule hiyo na kuwasisitiza kutunza miti iliyopandwa pamoja na mazingira kwa ujumla.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Katibu tawala wa Wilaya hiyo Bw. Bahati Mfungo ameipongeza NCAA kwa ushirikiano inaotoa kwa wananchi wa Wilaya ya Karatu hasa kuwapa elimu ya mazingira, upandaji miti, kupambana na mgongano kati ya Wanyamapori na wananchi pamoja na kusaidia miradi mbalimbali ya wananchi ikiwemo huduma za kijamii.

Siku ya Askari wa Wanyamapori Duniani ilianza kuadhimishwa mwaka 2007 kwa lengo la kuwakumbuka askari waliopoteza maisha wakati wa kutekeleza majukumu yao, kauli mbiu ya maashimisho ya mwaka huu ni “ Rangers: Powering Transformative Conservation”  ikilenga kuutambua mchango wa askari wa Wanyamapori katika kuleta mabadiliko ya kweli katika uhifadhi wa maliasili ambayo ni urithi wa Taifa.

RAIS SAMIA AZINDUA USAFIRISHAJI WA MIZIGO KWA TRENI YA UMEME (SGR) KUTOKA DAR HADI DODOMA




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 30 Julai 2025, ameandika historia mpya kwa kuzindua rasmi usafirishaji wa mizigo kwa kutumia Treni ya Umeme ya SGR kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kupitia Kituo cha Kwala, mkoani Pwani.

Uzinduzi huu ni hatua kubwa ya maendeleo katika sekta ya uchukuzi, ukilenga kuboresha usafirishaji wa mizigo nchini kwa kutumia miundombinu ya kisasa, rafiki kwa mazingira na yenye kasi zaidi. Treni hii ya umeme inatarajiwa kupunguza muda wa kusafirisha mizigo, kupunguza gharama za usafirishaji, pamoja na kupunguza msongamano wa malori barabarani.

Akizungumza katika hafla hiyo ya uzinduzi, Mhe. Rais Samia amesema kuwa utekelezaji wa mradi huu mkubwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuhakikisha Tanzania inakuwa kitovu cha usafirishaji wa mizigo Afrika Mashariki na Kati.

“SGR ni mradi wa kimkakati. Leo tunashuhudia ndoto kubwa ya Watanzania ikitimia – mizigo sasa inasafirishwa kwa haraka, salama na kwa tija zaidi,” alisema Rais Samia.

Treni hiyo ya umeme inatarajiwa kuongeza ufanisi katika usambazaji wa bidhaa, kusaidia wakulima, wafanyabiashara na viwanda kwa kusafirisha bidhaa kwa bei nafuu na kwa wakati.

SERIKALI YAWATAKA WAKUU WA TAASISI ZA UMMA KUTENGENEZA MAZINGIRA RAFIKI YA KAZI










Kibaha, Pwani. Serikali imewataka wakuu wa taasisi za umma kutengeneza mazingira rafiki ya kazi yatakayowawezesha watumishi kuongeza tija na ubunifu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kauli hiyo ilitolewa na Mhe. Ridhiwani Kikwete, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, alipokuwa akifunga mafunzo elekezi ya siku nne kwa Watendaji Wakuu wa Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali - Kundi la Pili, Jumatano, Julai 30, 2025, katika Shule ya Uongozi ya Mwl. Julius Nyerere, Kibaha, Pwani.

Katika hotuba yake, Waziri Kikwete aliwataka wakuu wa taasisi za umma kusimamia vizuri rasilimaliwatu ikiwa wanataka kuongeza ufanisi wa taasisi wanazoziongoza.

“Ikiwa mnataka kupata matokeo mazuri, mnapaswa kuepuka kuwa miungu watu na badala yake tengenezeni mazingira mazuri ambayo yatawahamasisha watumishi kujituma, kuleta ubunifu na kuongeza tija katika kila ngazi ya utendaji,” alisema Mhe. Kikwete. 

Mhe. Kikwete aliendelea kwa kutoa angalizo, “Lakini simaanishi muwachekee wazembe. Ninachomaanisha ni nyie kufanya kazi kwa msukumo, weledi na kuzingatia misingi ya utawala bora.” 

Hii inamaanisha kuwa wakuu wa taasisi wanapaswa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na kuhakikisha kwamba kila mfanyakazi anahisi kuheshimiwa na kuwa na nafasi ya kutoa mawazo ambayo yataboresha huduma na kuleta mabadiliko chanya. 

Hii, alisema, ni njia ya kuhakikisha taasisi zinakuwa na tija kwa muda mrefu na kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia na kiutendaji.

Mageuzi yanayoendelea katika kuimarisha utendaji kazi na usimamizi wa Taasisi za Umma yameongeza uwezo wa Serikali kufaidika na uwekezaji wa Sh86.29 trilioni.

Hili linadhihirishwa na gawio la mwaka wa fedha 2024/25, ambapo Mhe. Rais. Dk. Samia Suluhu Hassan alikabidhiwa Sh1.028 trilioni kama mapato yasiyo ya kikodi kutoka kwa taasisi, Mashirika ya Umma, Wakala za Serikali na kampuni ambazo serikali ina umiliki wa hisa chache.

“Kiasi hicho ni cha kihistoria. Lengo letu la msingi ni kuhakikisha kuwa uwekezaji wa Serikali katika Taasisi na Mashirika ya Umma unaendelea kuleta tija kwa Taifa letu kwa mfumo endelevu,” alisema Mhe. Kikwete. 

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof Kitila Mkumbo, alisema kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina serikali itahakikisha inatengeneza mazingira ambayo yatapelekea kutimia kwa maono ya Mhe. Rais ya kujenga Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali imara na zenye uwezo wa kuharakisha kufikiwa kwa maendeleo ya Taifa letu.

Aidha, Prof Mkumbo alisisitiza umuhimu wa utekelezaji wa miongozo ya serikali na sheria zinazohusu usimamizi wa taasisi, kwa lengo la kudhibiti matumizi yasiyo na tija na kuimarisha usimamizi wa rasilimali za umma kwa manufaa ya taifa.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais (Utumishi), Bw. Juma Mkomi, alisema mafunzo kwa wakuu wa taasisi, yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Msajili wa Hazina na Taasisi ya Uongozi, ni kitendea kazi kikubwa kwani yamegusa rasilimali watu.

Mafunzo hayo yaliyowaleta pamoja wakuu wa taasisi 114 yamewapa washiriki ujuzi na mbinu za kisasa za usimamizi, ikiwemo kuendeleza utamaduni wa uwajibikaji, uwazi, na ufanisi katika taasisi zao.

“Ni imani yangu mafunzo yataongeza ufanisi katika usimamizi wa rasilimali watu,” alisema Bw. Mkomi huku akiongeza kuwa, “kujifunza ni suala endelevu, msione haya kujifunza kutoka kwa wasaidizi wenu.”

“Ukijifunza kutoka kwao, wataona na wao ni sehemu ya uendeshaji wa taasisi na hivyo watafanya kazi kwa kujituma na ufanisi Zaidi.”

Kwa upande wake Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, alisema ili kufanikisha safari ya mageuzi ya mashirika ya umma, inahitajika uongozi thabiti, ubunifu, na mshikamano wa pamoja kati ya taasisi za umma, Wizara mama, Ofisi ya Msajili wa Hazina na wadau wengine wa serikali. 

Aliwahimiza watendaji wakuu kuendelea kujifunza na kubadilisha mtazamo wao ili kuendana na mageuzi ya utawala bora yanayohitajika kufanikisha maendeleo endelevu ya taifa.

“Tunaweza kuupata ufanisi wa matokeo chanya kama uongozi utakuwa na ufanisi,” alisema huku akiongeza kuwa Ofisi ya Msajili wa Hazina itaendelea kufanya mageuzi ili taasisi zilete tija iliyokusudiwa.

Wednesday, July 30, 2025

Rais Samia Kuzindua Usafirishaji wa Mizigo kwa SGR na Bandari ya Kwala















Na Mwandishi Wetu – MAELEZO, Kibaha - Pwani

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuzindua kuanza kwa huduma ya usafirishaji wa mzigo kwa njia ya SGR katika bandari Kavu ya Kwala, Kibaha mkoani Pwani pia kuzindua kongani ya viwanda ambayo itakua na viwanda zaidi ya 200 mkoani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukagua maandalizi ya uzinduzi huo katika eneo la Bandari Kavu ya Kwala, Kibaha Pwani , Julai 30, 2025, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge amesema uzinduzi huo utaambatana na upokeaji wa mabehewa ya treni ya SGR na upokeaji mabehewa ya mizigo ya treni ya MGR. 

Mhe. Kunenge amesema uwekezaji huo mkubwa ni matokeo ya maono na miongozo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo yamewezesha kuweka mazingira wezeshi ya kisera kwa sekta ya viwanda na biashara akibainisha kuwa matarajio ya Serikali ni kupunguza msongamano wa makasha katika bandari ya Dar es Salaam kwa asilimia 30 pia msongamano wa malori kwenye barabara ya kuu inayoelekea mkoani Morogoro na ile ya TANZAM.

Ameongeza kuwa mradi huo utaongeza ajira kwa Watanzania, kukuza ukusanyaji wa mapato ya kodi na kuboresha ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini akibainisha kuwa eneo hilo lina nafasi ya kipekee kijiografia kutokana na kuunganishwa na miundombinu mbalimbali ya usafirishaji, jambo linalotarajiwa kuchochea biashara ya kimkakati kati ya Tanzania na nchi jirani.

“Bandari kavu ya Kwala imezungukwa na bandari kavu za nchi  takribani 11 zinazotumia Bandari ya Dar es Salaam zikiwemo Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Malawi na nyingine za maziwa makuu ambazo tayari zina maeneo hapa, Kwala imeileta Jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi za SADC hapa" amesema Mhe. Kunenge.

Mhe. Kunenge ametoa wito kwa wananchi wajitokeze kwa wingi katika hafla ya uzinduzi huo itakayofanyika Julai 31, 2025 akibainisha kuwa kongani ya viwanda na bandari kavu ya Kwala itakuwa na manufaa makubwa katika uchumi wa wananchi kupitia ajira na shughuli za ujenzi na usafirishaji.

RAIS SAMIA AZINDUA KIWANDA CHA MAJARIBIO CHA UCHENJUAJI MADINI YA URANI MKOANI RUVUMA









Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Julai 30, 2025, ameweka historia kwa kuzindua rasmi Kiwanda cha Majaribio cha Uchenjuaji wa Madini ya Urani kilichopo Wilaya ya Namtumbo, Mkoa wa Ruvuma.

Akibonyeza kitufe maalum kuashiria uzinduzi huo, Rais Samia amesema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuhakikisha madini yote nchini, ikiwemo urani, yanachakatwa hapa hapa nchini kwa manufaa ya Watanzania wote. Ameongeza kuwa kiwanda hiki kitasaidia kuongeza thamani ya madini, kutoa ajira kwa wananchi wa maeneo husika, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kitaifa.

Uwekezaji huu ni sehemu ya mpango mpana wa kukuza sekta ya madini kwa njia endelevu na salama, huku Serikali ikidhamiria kuhakikisha usimamizi bora wa rasilimali za taifa unawanufaisha Watanzania wa sasa na vizazi vijavyo.

Wananchi wote wanahimizwa kuendelea kufuatilia taarifa rasmi na matukio mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii:

📍 Instagram: @mamakajatz
📍 Twitter/X: @mamakajatz
📍 Facebook: Mama Kaja TZ
📍 YouTube: Mama Kaja TZ

#MamaKaja #KaziIendelee #MadiniNiMaendeleo #TanzaniaYaViwanda

*WAZIRI MKUU AKAGUA MABASI, MIUNDOMBINU YA MRADI WA BRT AWAMU YA PILI

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Agosti 13, 2025 amekagua mabasi mapya kwa ajili ya awamu ya pili mradi wa mabasi yaendayo haraka (BRT-2) pa...