Tuesday, August 24, 2010

CUF yapata pigo wagombea wawili wafa


Wagombea wawili wa Chama cha Wananchi (CUF) wamefariki dunia jana visiwani Zanzibar katika matukio tofauti.Waliofariki dunia ni alikuwa Mwakilishi wa Jimbo la Kojani (CUF), Omar Ali Jadi (55) Mkoa wa Kaskazini Pemba na Mwalimu Shani Hamada Shani ambaye ni mgombea wa udiwani wa chama hicho katika Jimbo la Kikwajuni. Jadi alikuwa akiugua ugonjwa wa kisukari na kwamba alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya figo. Shani alifariki dunia baada ya kugongwa na gari wakati akielekea kuchukua fomu katika Tume ya Uchaguzi Zanzibar(ZEC), eneo la Maisara.Habari ya Salma Said, Zanzibar. SOURCE: CUF

No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...