Sunday, July 05, 2009

Uchaguzi Biharamulo





Wananchi katika Jimbo la Biharamulo Magharibi mkoani Kagera leo wanapiga kura kumchagua mbunge wao baada ya kampeni za uchaguzi huo kukamilika jana huku ushindani ukitarajiwa kuwa mkali kati ya vyama vya Chadema na CCM.

Leo wanapiga kura kumchagua mbunge wao baada ya kampeni za uchaguzi huo kukamilika jana huku ushindani ukitarajiwa kuwa mkali kati ya vyama vya Chadema na CCM.

Katika uchaguzi huo, ambao kampeni zake zilitawaliwa na vurugu, kila chama kilifanya kampeni ya nguvu kutupa kete yake ya mwisho kujinadi kwa wapigakura.

CCM ilihitimisha kampeni zake Biharamulo mjini katika Uwanja wa Sokoni, huku Chadema ikihitimisha kampeni zake katika uwanja wa mpira mjini hapa.

Wanaochuana ni Dk Anthony Gervas Mbassa wa Chadema, Oscar Rwegasira Mukassa wa CCM na Mpeka Buhangaza wa TLP.

Katika uchaguzi huo vituo 238 vimetengwa kwa ajili ya kupigia kura na waliojiandikisha kupiga kura ni watu 87,189.


Lwakatare naye yumo Chadema.

No comments:

TANZANIA NA URUSI ZAIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI KATIKA SEKTA YA UCHUKUZI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Shirikisho la Urusi zimeingia hatua mpya ya ushirikiano wa maendeleo baada ya kus...