Friday, July 31, 2009

Majambazi yakupua mamilioni NMB Dar



Majambazi yaliyotumia gari zilizokuwa na nambari za usajili zinazofana na za magari ya serikali kuvamia benki ya Benki ya NMB tawi la Temeke mida ya saa tano na dakika 13 asubuhi ya leo, kufanya mashambulizi na kupora fedha zaidi ya Sh150 milioni.

Katika heke heka hizo majambazi hayo yalimuua mlinzi mmoja, kuwajeruhi watu zaidi ya kumi wengine wakiwa mahututi waliokimbizwa hospitali Temeke na Muhimbili.

Majambazi hao walifika wakiwa na silaha kali pamoja na mabomu mengine yakiwa kwenye vifuu vya nazi walikuja na magari mawili moja yenye namba za usajili STJ aina ya Prado yenye rangi ya kijani na Vitara yenye namba SU.

Walianza mashambulizi katika kibanda cha mlinzi kwa kupiga risasi hovyo iliyowajeruhi askari na kuamua kurusha bomu lililomfikia mlinzi wa benki hiyo aliyetambulika kwa jina la Seif Mwikwike wa kampuni ya Moku Security Service iliyomjeruhi vibaya katika maeneo ya kichwani, kifuani na mguuni na kupoteza maisha yake.

Hali ya mashambulizi yaliendelea wakati majambazi hao walipoingia ndani ya benki hiyo kwa kuanza kuwajeruhi baadhi ya watunza fedha (Cashiers) kwa kurusha bomu lingine ambalo lilimjeruhi mhasibu iliyosababisha kusambaa kwa damu ndani ya benki. Taarifa kwa mujibu wa Felix Mwagara wa Mwananchi