Friday, July 17, 2009

Mdigrii



kwa waliowahi kusoma hapa mlimani nadhani watakuwa wanaufahamu vizuri mti huu maarufu kama MDIGRII. Chini ya mti huu vichwa vilikuwa vikiumia na mambo mengi wakati huo hakika nimeukumbuka mdigrii, hivi sasa ndivyo unavyoonekana mti huu kama ulivyokutwa na mdau wetu, zamani tulikuwa tukibeba viti baadaye vikajengwa vijiwe tulivyovifahamu kama VIMBWETE kutokana na umaarufu wa aliyeanzisha mpango wa mabadiliko ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Professa Tolly Mbwete ambaye wakati huo alikuwa kitivo cha Uhandisi sasa ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

No comments:

MSAJILI WA HAZINA AZINDUA MPANGO MKAKATI WA NMB 2026-2030

Mwandishi wa OMH Dar es Salaam. Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, amezindua Mpango Mkakati wa Muda wa Kati wa Benki ya NMB wa mwaka...