Friday, July 17, 2009

Mdigrii



kwa waliowahi kusoma hapa mlimani nadhani watakuwa wanaufahamu vizuri mti huu maarufu kama MDIGRII. Chini ya mti huu vichwa vilikuwa vikiumia na mambo mengi wakati huo hakika nimeukumbuka mdigrii, hivi sasa ndivyo unavyoonekana mti huu kama ulivyokutwa na mdau wetu, zamani tulikuwa tukibeba viti baadaye vikajengwa vijiwe tulivyovifahamu kama VIMBWETE kutokana na umaarufu wa aliyeanzisha mpango wa mabadiliko ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Professa Tolly Mbwete ambaye wakati huo alikuwa kitivo cha Uhandisi sasa ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

No comments:

TANZANIA NA URUSI ZAIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI KATIKA SEKTA YA UCHUKUZI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Shirikisho la Urusi zimeingia hatua mpya ya ushirikiano wa maendeleo baada ya kus...