Friday, July 17, 2009

Mdigrii



kwa waliowahi kusoma hapa mlimani nadhani watakuwa wanaufahamu vizuri mti huu maarufu kama MDIGRII. Chini ya mti huu vichwa vilikuwa vikiumia na mambo mengi wakati huo hakika nimeukumbuka mdigrii, hivi sasa ndivyo unavyoonekana mti huu kama ulivyokutwa na mdau wetu, zamani tulikuwa tukibeba viti baadaye vikajengwa vijiwe tulivyovifahamu kama VIMBWETE kutokana na umaarufu wa aliyeanzisha mpango wa mabadiliko ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Professa Tolly Mbwete ambaye wakati huo alikuwa kitivo cha Uhandisi sasa ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

No comments:

KAMISHNA BADRU ATAKA UBUNIFU ILI KUENDELEZA MAPANGO YA AMBONI

KAMISHNA BADRU ATAKA UBUNIFU ILI KUENDELEZA MAPANGO YA AMBONI  Na Hamis Dambaya, Amboni Tanga. Kamishna wa Uhifadhi Mamlaka ya Hifadhi ya Ng...