Friday, July 17, 2009

Mdigrii



kwa waliowahi kusoma hapa mlimani nadhani watakuwa wanaufahamu vizuri mti huu maarufu kama MDIGRII. Chini ya mti huu vichwa vilikuwa vikiumia na mambo mengi wakati huo hakika nimeukumbuka mdigrii, hivi sasa ndivyo unavyoonekana mti huu kama ulivyokutwa na mdau wetu, zamani tulikuwa tukibeba viti baadaye vikajengwa vijiwe tulivyovifahamu kama VIMBWETE kutokana na umaarufu wa aliyeanzisha mpango wa mabadiliko ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Professa Tolly Mbwete ambaye wakati huo alikuwa kitivo cha Uhandisi sasa ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

No comments:

Prof. Mfaransa Aja na Kitabu: Aiambia Dunia Kutalii Tanzania ni Tiba

Na Mwandishi Wetu Paris, Ufaransa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, akiwa nchini Ufaransa jana Julai 8, 2025 amek...