Tuesday, July 14, 2009

Msitu wa Nyumbanitu




Kijiji cha jadi cha Nyumba Nitu kilichopo Kata ya Mdandu Wilaya ya Njombe. Kijiji hiki ni muhimu sana kwa utalii na ni muhimu sana kwa utunzaji wa mimea na hifadhi ya mazingira.
Msitu huu ni wa maajabu sana kwani miti yake na mimea yake iko pale kwa karne nyingi na hata wanafunzi wetu wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine huenda pale kwa kujifunza aina za mimea.
Mbali ya msitu kuna kuku weusi wa ajabu na kuna mapango makubwa pale Nyumbanitu ambayo watu zaidi ya mia moja wanaweza kuishi kwenye mapango hayo yalikuwa yanatumika wakati wa vita. Maajabu hayo ni sawa kabisa kama yalivyo nchini Japan. Picha imepigwa na mdau Tumaini Msowoya aliyekuwapo ndani ya msitu huo kwa siku nzima amenieleza mambo mengi kuhusu msitu huu si mchezo.