Sunday, July 05, 2009

Matokeo Biharamulo

MATOKEO ya awali ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Biharamulo Magharibi yameonyesha Chama cha Chadema kikikaba koo chama cha CCM kwa kura chache ambazo hata hivyo zinaweza kufikiwa na CCM.

Mpaka sasa asilimia 84 ya kura zimeshahesabiwa na matokeo yanaonyesha kuwa Chadema kimezoa asilimia 51.2 ya kura zote huku CCM kikipata asilimia 48.8 ya kura na TLP kimiambulia asilimia 0.65. Matokeo haya ni ya awali na hayajathibitishwa na tume ya uchaguzi.

Matokeo kamili yatatolewa kesho hivi sasa wanakusanya masanduku ya kura na matokeo kutoka bush na vyama vimekubaliana matokeo kesho. Tofauti na uchaguzi uliopita, matokeo ya uchaguzi wa Jimbo la Biharamulo yamekuwa ni ya kushangaza, kwani katika maeneo ya vijijini ambako ndiko kunakotarajiwa kuwa ngome ya chama tawala cha CCM baadhi ya kata zinaonyesha kuwa na kura nyingi za mgombea wa Chadema.

Lakini pia maeneo ya mijini ambayo yanaonekana kuwa ni ngome kubwa ya vyama vya upinzani, lakini kwa Biharamulo CCM ilionekana kuchuana vikali katika vituo na kata mbalimbali huku vituo vingine vyama hivyo vikilingana kwa kura. Matokeo kamili tutawaletea kesho.

1 comment:

Anonymous said...

The rudimentary to this treatment is the low intensiveness laser rays directed to
the cellulites of cellulite so you can in reality cut 5-7 inches of your
consistency. Collagen: You can facilitate you pelt's snap by adding foods that comprise vitamin C can feature a better melodic theme on these ingredients. De-hydrated cells go washy and intelligent material and commence overcoming in few years. This is an alternative handling which doesn't take you be at the details depressed infra if you would like to
know.

My blog post: best anti cellulite cream