Thursday, May 21, 2009

Dk Mwakyembe apata ajali mbaya


MBUNGE wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe amepata ajali mkoani Iringa karibu na eneo la Mafinga akiwa njiani akitoka Kyela kuelekea jijini Dar es Salaam, walioshuhudia tukio hilo wanaeleza kuwa gari la Dk Mwakyembe lilipata ajali baada ya kukwepa lori na kisha kutumbukia katika korongo ambapo tairi lilichomoka gari limeharibiwa vibaya na Dk Mwakyembe mwenyewe amekimbizwa hospitalini ambapo anaendelea na matibabu na anaweza kuzungumza kama, lakini haijajulikana ni kiasi gani ameumia.

Tutaendelea kuwaleteeni taarifa zaidi kadri muda unavyokwenda kuhusiana na maendeleo ya kiafya ya Dk Mwakyembe, ambaye amejitokeza siku za karibuni kukabiliana vikali katika vita dhidi ya ufisadi, vita vilivyomuingiza katika malumbano makali na wana- CCM wenzake pamoja na baadhi ya wafanyabiashara.

No comments:

VIONGOZI WAKUU WA SERIKALI WAPIGA PICHA YA PAMOJA BAADA YA KIKAO CHA MWISHO CHA BARAZA LA MAWAZIRI AWAMU YA SITA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza kikao cha mwisho cha Baraza la Mawaziri cha Serikali...