LEO itakuwa mwisho kwa jina la Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Kapteni George Mkuchika, kutajwa katika vyombo vya habari baada ya Wahariri kuamua kutoandika au kutangaza habari zake katika vyombo vya habari.
Wahariri wa vyombo vya habari nchini, wameamua kwa pamoja kususia kuandika habari zote zinazomuhusu waziri huyo kupinga hatua yake ya kulifungia gazeti la MwanaHalisi kutochapishwa kwa miezi mitatu..
Kauli hiyo ya pamoja, ilitolewa jana na Jukwaa la Wahariri nchini, katika mkutano wao uliofanyika katika Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam na kutoa maamuzi yao juu ya kufungiwa kwa gazeti hilo bila ya kupewa muda wa kutosha kujitetea kuhusiana na walichokiandika.
Pamoja na uamuzi wa kutoandika habari za waziri huyo, pia wahariri hao wameamua, kufungua kesi ya kupinga kufungiwa kwa gazeti hilo, na kufanya maandamano siku ya Ijumaa kwa lengo la kuelezea kero zao na kuziandikia barua nchi wafadhili kuelezea jinsi Tanzania inavyoanza kuingilia uhuru wa vyombo vya habari.
Na Festo Polea
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA AMALIZA ZIARA YA SIKU MOJA MKOANI MBEYA
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), leo ameondoka Mkoani Mbeya baada ya kukamilisha zi...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
No comments:
Post a Comment